• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

'Marufuku ujenzi bila kibali' - Lukuvi

Imewekwa tarehe: January 14th, 2020

ONYO hilo limetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, alipokuwa akizungumza na wananchi wa mtaa wa Ndachi Kata ya Mnadani katika ziara yake ya kutembelea eneo hilo na eneo la Nkuhungu Broad Acer, jijini Dodoma.

Akikagua nyumba zilizojengwa kwenye eneo hilo bila vibali, alisema jambo hilo halitakubalika na sheria inaruhusu kubomoa nyumba za aina hiyo.

Aidha, waziri huyo aliweka alama ya X kwenye nyumba ambazo wamiliki wa viwanja wameanza ujenzi bila kuwa na vibali kutoka Ofisi ya Ardhi ya jiji hilo, na kuamuru kusitisha ujenzi huo.

Akiwa katika eneo hilo alimpigia mmoja wa wamiliki ambaye ni mtumishi wa umma ambaye mafundi walikutwa wakiendelea na ujenzi bila vibali.

“Ninataka nione hati yako, kibali cha ujenzi, unajua mtumishi wa umma hujengi mahali hadi uwe umemiliki na kupewa kibali cha ujenzi na Manispaa, kwanini umeamrisha pajengwe,” alihoji.

“Samahani waliniambia huku hawana vibali kwa kuwa ni pembezoni mwa mji,” alijibu dada huyo na waziri kusema: “Sheria haijasema pembezoni mwa mji watu wajenge tu, sasa usiendelee kujenga nasimamisha leo, mwambie fundi wako aache kujenga na ujenzi hadi upate kibali.”

Akizungumza na wananchi hao, alisema: “Mtu yeyote anayejenga mjini mahali popote bila kufuata utaratibu wa kumilikishwa yaani kiwanja ambacho hakijapimwa, hujamilikishwa, huna kibali cha wenye mamlaka ya mji unaohusika ujue unajipeleka kwenye hatari ya kuvunjiwa na kuondolewa jengo lako.”

“Msinijaribu na msimjaribu Mahenge (Mkuu wa Mkoa wa Dodoma), sisi serikali tuna nguvu, ole wenu tukute vyoo vinajengwa, mapagale yanajengwa tutayavunja, tumeshavumilia vya kutosha,” alisema.

Kwa mujibu wa Lukuvi, kila anayejenga hata kama ana pagale au msingi serikali itatafuta namna ya kumilikisha, na kwamba kwa sasa wanatakiwa kuacha wapime zipatikane barabara, viwanja vya watoto na ndipo umilikishaji uendane na ukubwa wa viwanja, na ujenzi waanze baada ya kupata vibali.

“Urasimishaji unaofanyika sasa ni huruma ya Rais, lakini kwa sheria ilitakiwa ni marufuku kuwabariki watu waliojenga kwa kuvunja sheria bila vibali, Rais aliniagiza waliotoa jasho lao wakajenga mjini wasivunjiwe ndiyo maana tunarasimisha makazi,” alisema.

Aidha, Waziri Lukuvi alisema serikali haina mpango wa kubomoa nyumba za wananchi isipokuwa wanatakiwa kujenga kwa kufuata utaratibu ikiwa ni pamoja na kupata kibali cha ujenzi.

Wakati huo huo, Waziri Lukuvi amefanikiwa kutatua mgogoro wa ardhi kwa wakazi wa Ndachi jijini Dodoma uliodumu kwa takribani miaka 14.

Aidha, ametoa miezi mitatu kwa Halmashauri ya Jiji, Idara ya Ardhi Mipango Miji na Rasilimali Watu kuhakikisha wanakamilisha upimaji na urasimishaji katika eneo hilo.

Alisema mgogoro huo umedumu kwa muda mrefu na kwamba serikali imeamua kuumaliza kwa kurasimisha wananchi waliojenga kiholela na kupima maeneo yote ambayo hayajapimwa.

Aidha, Waziri Lukuvi baada ya kusikiliza wananchi na kupitia hati zao ilibainika kuwa asilimia kubwa ya hati zimemaliza muda wake wa miaka 33 tangu zitolewe mwaka 1985, na kusisitiza kuwa kwa sasa ardhi hiyo siyo mali yao bali ni mali ya Rais hivyo irejeshwa kwake kwa matumizi yanayotolewa mwongozo upya.

ONYO KWA WANANCHI WAKOROFI

Aliwaonya wananchi wa eneo hilo wenye tabia ya kutumia silaha kama mapanga na mishale na kuzuia watumishi wa serikali kufanya kazi yao kuacha tabia hiyo mara moja.

"Ninyi mnaojifanya mnajua kutumia silaha za upinde, mishale, sime na mapanga, muache tabia hiyo mara moja, maana serikali ina silaha za moto… sasa ole wenu muwazuie watendaji wa Jiji kufanya kazi yao ya upimaji na kuchelewesha kazi hiyo, tutawashughulikia barabara," alisema Lukuvi.

Alisema baada ya wananchi hao kupimiwa, watalipa gharama za kodi ya serikali zitakazokuwa zimepangwa na kuruhusiwa kuanza ujenzi au kuendelea na ujenzi.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.