• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Matumizi sahihi ya TEHAMA, yachochee maendeleo ya mtoto wa kike

Imewekwa tarehe: October 12th, 2021

MATUMIZI sahihi ya digitali kwa mtoto wa kike yatachochea maendeleo endelevu kupitia nyanja za elimu, biashara, habari na mawasiliano nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Aziza Mumba katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani yaliyofanyika ngazi ya wilaya katika Kata ya Nkuhungu jijini Dodoma.

Mumba alisema kuwa matumizi sahihi ya digitali kwa mtoto wa kike yatachochea maendeleo katika nyanja za elimu, biashara, siasa, habari na mawasiliano. “Hii itapelekea maendeleo endelevu katika jamii kwa kupata wataalam wa nyanja mbalimbali na pia kuzalisha ajira rasmi na zisizo rasmi. Hali hii itachochea mtoto wa kike kujiongezea kipato na kuwajengea uwezo, ujasiri katika kufanya maamuzi sahihi. Ikumbukwe kwamba mtoto wa kike ni mama mtarajiwa hivyo, kumjengea uwezo wa kujiamini ni kujenga jamii inayojiamini na kujisimamia” alisema Mumba.

Mwakilishi huyo wa Katibu Tawala wa Mkoa, ambae pia ni Katibu Tawala Msaidizi anayesimamia sekta ya Uchumi na Uzalishaji katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alisema matumizi sahihi ya digitali yamlinde mtoto dhidi ya madhara yanayoweza kutokea. “Nitoe rai kwa jamii kutumia vizuri digitali ili kumwepusha mtoto wa kike na madhara yanayoweza kutokea iwapo haitatumika vizuri. Madhara hayo ni kama unyanyasaji wa kijinsia, mimba za utotoni, kutumia muda mwingi katika vyombo vya kidigitali na kushindwa kuzalisha na pia kumomonyoka kwa maadili katika jamii” alisema Mumba.

Aidha, aliwataka kuzipuuza mila na tamaduni za kigeni ambazo ni kinyume na maadili ya kitanzania na kuwataka kudumisha mila nzuri za kitanzania zinazolinda heshima, utu na ubinadamu. “Maana siku hizi kumeibuka tabia za kuiga katika mitandao ya kijamii mambo yasiyofaa na yenye kudhalilisha utu na ubinadamu wetu. Tabia hizi tuachane nazo kwa sababu hazitusaidii na badala yake zinasababisha mmommonyoko wa maadili katika taifa” alisema Mumba.

Akimkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Asha Vuai alisema kuwa lengo la maadhimisho hayo ni kuwaelimisha na kuwakumbusha wazazi umuhimu wa mtoto wa kike katika kipindi hiki cha kidigitali.

“Kama ujumbe unavyosema ‘Kizazi cha Kidigitali ni kizazi chetu’ Tutumie vifaa vya TEHAMA kwa lengo la kuelimisha watoto kama kufanya ‘homework’ na kujifunza. Tuangalie watoto wanapojifundisha ili wasijifundishe mambo ya ajabu. Tunaona mimba za utotoni zimekuwa tatizo kubwa sababu ni watoto wanajifundisha mambo mabaya kupitia TEHAMA” alisema Viai.

Aidha, aliwataka wazazi kuhakikisha wanawalea watoto wao na kuwa nao makini ili TEHAMA iwe msaada katika kuwafundisha na kuwalea watoto.

Maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike duniani yamefanyika ngazi ya wilaya ya Dodoma katika Kata ya Nkuhungu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.