• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mavunde achochea moto ujenzi wa sekondari

Imewekwa tarehe: June 17th, 2020

Wakazi wa Kata ya Chahwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kuhakikisha wanawapeleka watoto shule kupata elimu kwani elimu ndio mkombozi wa maisha yao, lakini pia kutailetea Kata hiyo maendeleo pamoja na Taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira, na Wenye ulemavu Mhe. Anthony Peter Mavunde alipokua akikabidhi vifaa vya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Chawa, ambayo imeanza kujengwa kwa nguvu za wananchi wa Kata hiyo, vifaa hivyo ni pamoja na mifuko 100 ya saruji, mchanga trip 6 na kokoto trip 3 huku akiahidi kutoa tofali elfu tano ili kufanikisha ujenzi huo, Mavunde amefanya hili ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa baada ya wananchi wa kuwasilisha maombi yao kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni alipokuwa akisikiliza kero za wananchi mwezi Januari 2020.

Mavunde amewapongeza wananchi hao kwa kujitoa, na kuamua kutumia nguvu zao kuanzisha ujenzi wa Sekondari hiyo, na yeye yupo tayari kuwasaidia kuona malengo yao yanatimia, na amewahakikishia kuwa mpaka kufikia Mwaka 2021 atakua amesimamamisha moja ya majengo ya Shule hiyo na wanafunzi wataanza kulitumia.

“Shule hii ni ya Wananchi, sitaki ionekane kuwa ni ya Mbunge, shule hii ni ya kwenu, nyinyi ndio wahusika wakubwa, muipende, muijali na msaidie kila hatua, mimi kazi yangu ni kuchochea maenedeleo tu lakini shule hii ni ya kwenu, kila mtu achangie hata kama una elfu tano usiione ndogo inaweza kusaidia kufanikisha ujenzi wa shule hii, Leo tunaandika historia mpya kwa kuanza kutatua kero ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata shule” alisema Mavunde.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Diwani aliyemaliza muda wake Mhe. Sospeter Mazengo amemshukuru Mhe. Mavunde kwa mchango mkubwa alioutoa katika ujenzi wa shule hiyo na kuwa historia itamkumbuka kwa kuchochea maendeleo kupitia  elimu ambapo shule hii itawasaidia wanafunzi wengi wanaotembea umbali mrefu kwa sasa ili kupata elimu kwa kusoma katika kata za jirani.

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Mwl. Happy Rweyemamu amewashukuru wananchi hao kwa kujitoa kwani wameonesha ni jinsi gani wanathamini elimu na wao kama Serikali wapo tayari kuwaunga mkono kwa kila namna kuhakikisha shule hiyo inakamilika.

“Ninajua kiu yenu kwasababu nimesikia kwenye ripoti iliyosomwa hapa, kuwa mnatamani 2021 wanafunzi wawe wameanza kuitumia shule hii, mimi kama kiongozi ninaesimamia elimu ya sekondari nitahakikisha shule hii inasajiliwa na inaanza kama nyinyi mnavyotamani iwe, pia nichukue nafasi hii kumpongeza Mhe. Mbunge, niwahakikishie tuna mbunge mzuri mchapakazi anaejituma na kujali wananchi wake” alisisitiza Mwl. Rweyemamu.

Mheshimiwa Anthony Mavunde (katikati) akifurahia jambo na Mkuu wa Idara ya Elimu ya Sekondari Upendo Rweyemamu wakati alipokuwa akikabishi vifaa mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari katika Kata ya Chahwa. Kulia ni aliyekuwa Diwani wa Kata ya Chahwa kabla ya kuvunjwa rasmi Mhe. Sospeter Mazengo.



Mhe. Mavunde akishiriki kazi ya kuchimba msingi wa darasa la shule ya sekondari inayojengwa.

Diwani aliyemaliza muda wake Mhe. Sospeter Mazengo akishiriki kuchimba msingi wa ujenzi wa  majengo ya shule ya sekondari.

Mifuko 100 ya saruji iliyotolewa na Mhe. Mavunde ikishushwa kutoka kwenye gari.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.