• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mavunde agawa vishikwambi 700 kwa shule za msingi, DC asema ni mchapakazi!

Imewekwa tarehe: February 27th, 2020

Shule 10 za elimu ya msingi za serikali na binafsi jijini Dodoma zimenufaika baada ya kupatiwa Vishikwambi 700 ambavyo vitawawezesha wanafunzi wa Jiji la Dodoma kusoma na kujifunza ki-eletroniki kufuatia utekekezaji wa mradi wa ugawaji wa vishikwambi kupitia Shirika la PROFUTURO pamoja na DON BOSCO.

Akimuwakilisha Mgeni Rasmi Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe. Patrobas Katambi amempongeza Mbunge Anthony Mavunde kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo katika kutatua changamoto za Elimu, na kuwataka wanafunzi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kusoma kwa bidii ili kuunga mkono juhudi za mbunge wao Mhe. Anthony Mavunde. Aidha, amezitaka shule zilizopata vishikwambi hivyo kuvitunza na kuvitumia kuchochea ufaulu kwa wanafunzi wao.

Katambi amesema kuwa wanafunzi wanatakiwa kusoma kwa bidii ili kujikwamua kielim. "Ndugu zangu wanafunzi, msichezee elimu mnayoipata kwa sababu ndiyo urithi wetu wa maana ya kipekee hapa duniani. Msiwekeze kwenye anasa na mapenzi muwapo shuleni" alisisitiza Mkuu huyo wa Wilaya.

"Tangu nimekuja Dodoma kama Mkuu wa Wilaya, nimejifunza jambo kubwa kupitia wewe la kuwapenda wananchi wako sana na kuweka msisitizo mkubwa kwenye Elimu kama silaha ya kuwakomboa wanafunzi katika Jimbo lako. Hongera sana Mheshimiwa Mavunde kwa kuendelea kuboresha sekta ya Elimu ukishirikiana na wadau kama hawa PROFUTURO, Dodoma Jiji lazima iwe tofauti na majiji mengine kiteknolojia na wewe haya unayajibu kwa vitendo" Alisema Katambi.

Aliendelea kusema "kazi unayoifanya ni kubwa na yenye tija kwa wana Dodoma na Taifa kwa ujumla. Mimi ni mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini, ni sehemu ya ushuhuda wa uchapa kazi wa Mbunge Anthony Mavunde. Kwa kweli ni mbunge wa mfano, mwenye uongozi shirikishi na ninaridhika na kazi anayofanya mbunge wetu" alifafanua zaidi.

Kabla ya hapo wakati akimkaribisha mgeni rasmi, Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe. Anthony Peter Mavunde amelishukuru shirika la PROFUTURO kwa kuchangia maendeleo kwenye sekta ya Elimu Jimboni Dodoma kuunga mkono juhudi na mkakati wa kuigeuza Dodoma Jiji kama moja ya maeneo yenye matumizi makubwa ya Sayansi na Teknolojia ambapo wanafunzi watajifunza masomo yao ya kawaida ya kwenye mtaala ki-eletroniki.

Awali akitoa maelezo ya mradi, Mwakilishi wa Shirika la PROFUTURO na Don Bosco Net Padri Peter Mutechura ameelezea namna ambavyo Shirika hilo limejikita kutoa huduma katika kuboresha sekta ya elimu kupitia Teknolojia na kuahidi kuendelea kushirikiana na Mbunge Mavunde kutatua changamoto mbalimbali za Elimu katika Jimbo la Dodoma Mjini.

Shule za msingi 10 zilizopewa vishikambi ni shule za msingi za Mlimwa, Mbwanga, Ihumwa, Chigongwe na Mazengo. Nyingine ni Brother Martin, Misericodia, Maria De Mattias, Chemchem na Capital.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.