• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mavunde ahimiza kasi ya utekelezaji miradi ya umeme Jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: April 24th, 2021

MBUNGE wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde ameitaka TANESCO pamoja na Mkandarasi wa Mradi wa Ujazilizi (Densification) Kampuni ya Derm Electrics kuongeza kasi ya usambazaji wa huduma ya nishati ya umeme ili kuyafikia maeneo mengi Zaidi ambayo bado hayaunganishwa na umeme Jijini Dodoma.

Mbunge Mavunde ameyasema hayo leo katika ukumbi wa Jiji la Dodoma wakati wa kikao baina ya TANESCO, Kampuni ya Derm Electrocs na Madiwani wa Jiji la Dodoma ambao maeneo yao yanaguswa na mradi wa Ujazilizi wa Umeme pamoja na mradi mwingine wa PERI URBAN.

Akitoa maelezo ya awali Meneja wa TANESCO Kanda ya Kati Ndugu Frank Chambua amewahakikishia viongozi juu ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi wa Ujazilizi wa Umeme na kwamba watamsimamia mkandarasi kufanya kazi ndani ya muda wake wa mkataba na ukiwezekana kazi kumalizika kabla ya muda wa mkataba wa mwaka mmoja ili wananchi wa Dodoma waanze kunufaika na huduma hiyo ya Nishati ya umeme kwa lengo la kuchochea maendeleo katika maeneo husika.

“Katika Kata 41 za Jimbo la Dodoma yapo baadhi ya maeneo ambayo bado hayajaunganishwa na nishati ya umeme, naishukuru Serikali kwa kututengea zaidi ya shilingi bilioni 100 kutekeleza miradi ya umeme mkoani Dodoma, ambao ikikamilika itaiwasha Dodoma yote na hivyo kuchochea maendeleo na ajira katika maeneo husika.

Pamoja na kazi nzuri anayofanya Mkandarasi Derm Electronics kuyafikia maeneo mengi ndani ya muda mfupi, ninawataka muongeze kasi zaidi ili wananchi wanufaike mapema na huduma hii ya nishati jambo ambalo naamini lipo ndani ya uwezo wetu” amesema Mavunde.

Akitoa neno la shukrani, Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Prof. Davis Mwamfupe amempongeza Mbunge Mavunde kwa namna ambavyo analisimamia suala la utekelezaji wa miradi ya umeme na kuwataka Madiwani kutoa ushirikiano kwa Mkandarasi na TANESCO wakati wa utekelezaji wa miradi hii ambayo italeta mageuzi makubwa katika Jiji la Dodoma.




   

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.