• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mbunge Mavunde afadhiri ujenzi wa darasa, Dkt. Mahenge ampongeza

Imewekwa tarehe: September 25th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amempongeza Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde kwa kasi ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM hasa katika Sekta ya Elimu kutokana na mchango mkubwa anaoutoa katika kuboresha miundombinu ya majengo ya shule na matundu ya vyoo katika Jimbo la Dodoma Mjini.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Mkuu wa Mkoa Dkt. Mahenge wakati wa uzinduzi wa darasa  lililojengwa kwa ufadhili wa Mbunge Mavunde kutokana na maombi ya Wananchi hao mwaka 2015 wakati wa Kampeni ya Uchaguzi ambapo kero kubwa iliyosemwa na wananchi ilikuwa ni upungufu wa madarasa katika Shule ya Msingi Chang'ombe B na Mbunge Mavunde kuahidi kuitatua pindi atakapochaguliwa.

"Wakati nakuja Dodoma nilikukuta una zoezi la kugawa matofali 32,000 na mifuko ya Saruji 3,200 kwa Kata zote 41 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na matundu ya vyoo, leo tena umeniita kwa jambo hili kubwa la kufungua Darasa. Unawatendea haki sana wananchi wako na Mungu akuongoze uendelee kuleta mabadiliko makubwa kwenye sekta ya Elimu" Alisema Dkt. Mahenge.

Akitoa salamu zake, Mbunge Mavunde ameeleza kwamba alianza utekelezaji wa ahadi yake hiyo mwaka 2016 kwa kuanza ujenzi huo polepole na kukamilika rasmi September, 2019 kwa gharama ya Tsh 15m (milioni kumi na tano) na hivyo kutatua changamoto hiyo ya upungufu wa vyumba vya madarasa ambapo awali wanafunzi walikuwa wanapata changamoto ya mazingira wezeshi ya kusomea.

Pamoja na darasa hilo, Mbunge Mavunde amekabidhi madawati 30 kwa ajili ya darasa hilo na pia ameanza ujenzi wa Ofisi ya walimu shuleni hapo huku akilipongeza Jiji La Dodoma kwa kutenga kiasi cha Shilingi Bilioni nane kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na miundombinu mbalimbali kwa Shule za Msingi na Sekondar Jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge (mwenye skafu shingoni), Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini Mhe. Anthony Mavunde (wa pili kushoto mbele) na Diwani wa kata ya Chang'ombe Mhe. Bakari Fundikira wakiongoza wananchi wa kata ya Chang'ombe, waalimu na wanafunzi kwenda kuzindua darasa lililojengwa kwa ufadhili wa Mbunge Mavunde.

Madarasa 30 (thelathini) yaliyotolewa na Mbunge Anthony Mavunde kutumika katika darasa aliloliljenga kutimiza ahadi yake wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 alipokuwa akijibu moja ya kero zilizokuwa zikiwasumbua wananchi wa kata ya Chang'ombe jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa Dkt. Binilith Mahenge akimpongeza Mbunge Anthony Mavunde kwa kasi kubwa ya kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi kuhusu uimarishaji wa Miundombinu ya Elimu.

Mbunge Anthony Mavunde (katikati) akifurahia pamoja na wanufaika wa darasa alilolijenga (wanafunzi) kwa ajili ya shule ya msingi Chang'ombe B.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.