• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Meya afurahishwa Idara kuunganisha wajasiriamali

Imewekwa tarehe: June 5th, 2020

MSTAHIKI Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe amefurahia ushirikiano wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana na Idara ya Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi kwa katika kuviunganisha vikundi vya wajasiliamali na kuvisaidia kukua kiuchumi.

Prof. Mwamfupe alisema kuwa ushirikiano wa idara hizo ni chachu kwa maendeleo. “Tunachokiona hapa ni ubunifu wa hali ya juu ya wataalam wetu. Katika hili tukio tunajifunza jambo moja kubwa kwamba hawa wataalam tukiwaamini, watajiamini. Nimekuwa nipenda ifeke hatua Jiji la Dodoma tunaboresha ufugaji wa watu wanaozunguka maeneo ya mji. Maeneo yao tumeyachukua kwa ajili ya maendeleo ya mji. Wananchi hao watafuga wapi kama wanamazoea ya ufugaji wa Ng’ombe wa kawaida wanaochukua maeneo makubwa” alihoji Mshahiki Meya.

Mstahiki Meya huyo alisema kuwa mpango wa halmashauri ni kugawa ngombe 150 kwa kipindi cha miezi 12 ijayo. Aidha, aliwataka vijana kuwa tayari kujikita katika sekta ya mifugo. “Vijana kaeni siyo mkao wa kula, najua mmeshana, njooni mle, tunafedha za kutosha, acha kufuga kwa ‘WhatsApp’ njoo jifunze, njoo ufuge. Kuna vijana wamemaliza vyuo njoo mfuge” alisisitiza Prof. Mwamfupe.

Akitoa maelezo mafupi ya hali ya ukopeshaji vikundi kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang’anya alisema kuwa vikundi vitano vinapatiwa Ng’ombe wa maziwa kutoka mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani ya halmashauri kwa vikundi vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. “Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, vikundi hivi ni baadhi tu ya vikundi ambavyo tumetoa mikopo kwa awamu hii. Mwaka huu wa fedha Halmashauri ya Jiji la Dodoma tumetoa shilingi bilioni 1.7 kwa vikundi mbalimbali. Vikundi hivyo vimenufaika kwa kutekeleza miradi ya aina mbalimbali. Vikundi hivi vitano viliamua kufanya shughuli ya ufugaji” alisema Nabalan’anya. 

Akiongelea upatikanaji wa Ng’ombe hao, Nabalang’anya alisema kuwa Idara yake kwa kushirikiana na Idara ya Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi walihakikisha kuwa fedha zinazoingizwa katika akaunti za vikundi hivyo zinaunganishwa pamoja na kuagiza Ng’ombe. “Ng’ombe hawa wametoka Arusha na wanathamani ya shilingi milioni 24. Ni Ng’ombe 12, kwa gharama ya manunuzi mpaka kuwafikisha hapa kila Ng’ombe amegharimu shilingi milioni mbili. Lakini jumla ya fedha ambazo vikundi hivi vimenufaika ni shilingi milioni 44, kwa hiyo bado kila kikundi kina kiasi cha fedha kwa ajili ya chakula, dawa na chanjo” alisema Nabalang’anya.

Kwa upande wa Afisa Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi Jiji la Dodoma, Gratian Mwesiga alisema kuwa Ng’ombe wanaogawiwa ni mitamba yenye mimba kati ya miezi sita hadi saba. “Umri wao ni kati ya miezi 18-22. Ng’ombe anauwezo wa kuzaa ndama 10 kwa maana maisha yake ya kuishi ni miaka 10. Hivyo, kila mwaka kama mambo yataenda vizuri atakuwa anazaa ndama mmoja mmoja” alisema Mwesiga. Aidha, alisema kuwa matarajio ya Halmashauri ni vikundi hivyo vifuge Ng’ombe hao kwa miaka 10. Vilevile, aliwataka wanavikundi hao kufuata ushauri wa wataalam wa mifugo ili kuweza kufuga kwa tija.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.