• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mfumo wa GePG wapaisha maduhuli ya Serikali

Imewekwa tarehe: September 17th, 2020

MFUMO wa Kielektroniki wa Ukusanyaji wa Mapato ya Kodi, Maduhuli, Tozo na Huduma (Government electronic Payment Gateway - GePG) umeongeza makusanyo ya maduhuli serikalini kwa asilimia 292 kutoka Sh bilioni 688.7 katika mwaka 2015/16 hadi Sh trilioni 2.699 mwaka 2019/2020.

GEPG pia imeboresha makusanyo katika taasisi 668 zilizojiunga likiwemo Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), ambalo ukubwa wake umeongezeka kwa asilimia 40 kutoka Sh trilioni 3.2 mwaka 2018 hadi Sh trilioni 4.8.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James (pichani) aliyasema hayo baada ya kupokea ripoti ya tathmini ya mfumo wa kieletroniki wa ukusanyaji mapato na usimamizi wa fedha, iliyoandaliwa na watalaamu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM).

James alisema GePG ni miongoni mwa mifumo minne mikubwa, ambayo imebuniwa na kutengenezwa na wazawa na kusimamiwa na Wizara ya Fedha na Mipango.

Mfumo mwingine ni wa Usimamizi na Udhibiti wa Matumizi na Malipo ya Serikali (MUSE), Mfumo wa Usimamizi wa Miradi ya Maendeleo (NPMIS) na Mfumo wa Usimamizi wa Misamaha ya Kodi.

Katibu Mkuu huyo alisema matumizi ya mifumo hiyo, yameleta mageuzi makubwa serikalini. Alitaka kila mtu anayelipa huduma ya umma, lazima apewe control namba na taasisi inayotoa huduma.

Pia alisema kila taasisi inayotaka kutekeleza mradi wowote wa maendeleo, lazima ihakikishe inatumia mfumo katika kufanya maombi ya kutekeleza mradi.

"Nasisitiza kwamba maafisa masuhuli wote kuhakikisha mnapata ridhaa ya Wizara ya Fedha na Mipango kabla ya kufanya ununuzi, uandaaji, usimikaji na matumizi ya mfumo wowote wa kielektoniki katika maeneo yenu," alisema James.

Akiwasilisha ripoti ya Tathmini ya Mfumo wa GePG, Mhadhiri Mwandamizi UDSM, Profesa Joel Mtebe alisema katika utafiti waliofanya kwa taasisi 271 katika kanda saba kwenye mikoa 11 kwa watendaji 384 na wakuu wa taasisi 257, asilimia 87 mfumo huo umesaidia kuongeza makusanyo ya maduhuli serikalini.

Profesa Mtebe alisema katika utafiti huo, asilimia 77 ya watumiaji wa mfumo huo wamesema ni bora na umesaidia kuongeza malipo ya serikali na asilimia 87 kati yao wamesema una ubora na asilimia 82 wamesema mfumo huo umeongeza uwezo wa serikali kukusanya maduhuli.

Katibu Mkuu alisema GePG ilianza kutumika Julai Mosi mwaka 2017 ili kukabiliana na changamoto serikalini zikiwemo za ukusanyaji fedha za umma, gharama kubwa za miamala iliyohusika makusanyo hayo, utararibu usio rafiki kwa mlipaji wa huduma na machaguo machache ya njia ya kulipia huduma.

Alisema mfumo huo umeleta faida 12 ikiwemo ya kuongeza uwazi na udhibiti makusanyo, upatikanaji wa taarifa sahihi za makusanyo na kwa wakati na pia kuchochea ubunifu katika ukusanyaji fedha na kutoa huduma bora na rahisi ya malipo.

"Fedha kufika haraka kwenye akaunti za makusanyo zilizopo Benki Kuu (BoT), kusaidia benki na mitandao ya simu kuwa na sehemu moja ya kuunganisha mifumo yao, kuwezesha benki na mitandao kuwa na mazingira rafiki na ya usawa katika uusanyaji fedha,”alisema Katibu Mkuu Hazina.

Pia kuzisaidia taasisi za umma kupunguza gharama zinazotokana na uwekezaji katika miundombinu ya Tehama, urahisi katika usuluhishi wa mialama na usuluhishi wa taarifa za kibenki, kupunguza gharama za miamala inayohusu ukusanyaji na kumuongezea mlipaji wa huduma machaguo mengi ya njia ya kulipia huduma za umma kama benki, wakala na mitandao ya simu.

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, William Erio alisema shirika hilo tangu limejiunga na GePG Aprili 2019, makusanyo ya kila mwezi yamepanda kutoka takribani Sh milioni 60 kwa mwezi hadi Sh milioni 100.

Erio alisema GePG imeleta mabadliko makubwa kwa shirika hilo katika ukusanyaji wa michango kutoka kwa wanachama wa sekta rasmi na isiyo rasmi na kwenye kodi ya pango katika vitega uchumi.

Tangu kujiunga na mfumo huo, NSSF imepunguza idadi ya akaunti ambazo zilikuwa zikitumika kutoka 78 hadi tatu, hivyo imekuwa rahisi kuweka hesabu sawa.

Mhasibu Mkuu wa Serikali, Francis Mwakapalila alisema kuanzishwa kwa Mfumo wa Usimamizi na Udhibiti wa Matumizi na Malipo ya Serikali (MUSE), kumepunguza gharama ambazo serikali ilikuwa ikitumia kulipia mifumo kutoka nje.

Mwakapalila alisema serikali kwa kutumia mfumo wa EPICA ilikuwa ikitumia Sh bilioni 5.6 kwa ajili ya kununua leseni na Sh bilioni 1.5 zilitumika kulipia uanachama na Sh milioni 500 kwa ajili ya kusaidia kuangalia mifumo hiyo inavyofanya kazi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.