• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mfumo wa GoTHOMIS wasimikwa Mkonze

Imewekwa tarehe: September 20th, 2021

Na. Getruda Shomi, DODOMA.

WAHUDUMU wa Kituo cha Afya Mkonze wameanza kupatiwa mafunzo ya mfumo wa kielektroniki wa huduma za afya (Government of Tanzania Health Management Information System - GoTHOMIS) utakaorahisisha kutunza kumbukumbu za wagonjwa na taarifa za malipo, utarahisisha kupatikana kwa historia ya mgonjwa na utoaji wa huduma kirahisi.

Mafunzo hayo yanatolewa na Afisa TEHAMA katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Caesar Faustine (pichani juu aliyesimama). Caesar alikuwa akitoa maelekezo ya namna ya kutumia mfumo huo wa kielektroniki kusajili wagonjwa, vipimo na namna ya ulipaji wa bili za matibabu.

Afisa TEHAMA huyo alisema “Serikali imeamua kuunda mfumo huu ili kuweza kurahisisha kazi kutoka kwenye kutumia mafaili hadi kwenye mifumo ya kielektroniki ambapo itasaidia kutunza kumbukumbu za wagonjwa na wagonjwa watapewa namba zao za kwenye mifumo ili wanapotaka tena kupata matibabu waweze kupatiwa kulingana na kumbukumbu za matibabu ya awali” alisema Faustine.

Wahudumu wa vituo vya afya watatumia mfumo huo kwa kutumia kompyuta ambazo zitawekwa kwenye kila kitengo cha matibabu kama vile mapokezi, maabara, maduka ya dawa, X-ray, na kadharika. Aidha, mfumo huo unauwezo wa kuchapa risiti za malipo.

Akizungumzia mfumo huo Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkonze, Dkt. Leticia Siwalima aliahidi kuwa watautumia vizuri kama walivyoelekezwa kwa sababu unalengo la kurahisisha kazi na kutunza kumbukumbu za wagonjwa.

“Mfumo huo ni mzuri na utasaidia kutunza kumbukumbu za wagonjwa, hivyo mpaka mwisho wa semina hii tutakuwa tumeweza kuutumia” alisema Dkt. Siwalima.

Naye Afisa TEHAMA John Longino alisema kuwa mafunzo na mazoezi ya utumiaji wa mfumo huo yanaendelea vizuri na wanamatumaini makubwa kuwa baada ya kukamilika kwa mafunzo na mazoezi, mfumo utaanza kutumia rasmi kuendesha shughuli za kila siku za utoaji huduma za afya kituoni hapo.

Hata hivyo, hadi sasa kituo kila kompyuta tano tu zilizounganishwa kwenye mfumo, wakati mahitaji halisi ni kompyuta 12. Tayari kituo kimeanza kuangalia namna ya kupata kompyuta zinazohitajika ambapo Kaimu Mganga Mfawidhi ameomba wadau kujitokeza ili kuchangia upatikanaji wa vifaa hivyo.

Ikumbukwe kuwa Mwenge wa Uhuru wa mwaka huu umebeba kauli mbiu isemayo ‘TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu, itumike kwa usahihi na uwajibikaji”. Hivyo basi, Jiji la Dodoma limejiwekea mikakati kuhakikisha kila kituo cha Afya na Zahanati inatumia mfumo wa kielektroniki ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.