• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mhe. Jafo azindua rasmi Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati Jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: August 7th, 2019

MAMLAKA za serikali za mitaa katika mikoa ya Dodoma na Singida zimetakiwa kuhakikisha mabanda yao yanakuwa ‘live’ katika uwanja wa maonesho wa Nanenane kwa kipindi cha mwaka mzima ili kutoa fursa kwa wananchi kujifunza na kuziongezea Halmashauri zao mapato.

Agizo hilo lilitolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Seleman Jafo alipokuwa akifungua rasmi maonesho ya Nanenane jijini Dodoma siku ya Jumanne 05 Agosti, 2019 katika viwanja vya Nanenane vilivyopo Nzuguni Jijini Dodoma.

Waziri Jafo alisema “nataka uwanja wa maonesho ya Nanenane uwe endelevu, usiwe uwanja mfu. Halmashauri zote hakikisheni mabanda ya Halmashauri yanakuwa ‘live’ mwaka mzima”. Kila Halmashauri imepata heka mbili, na kuzitaka kutengeneza miundombinu kwa ajili ya umwagiliaji wa njia ya matone. “Wekeni hapa ‘drip irrigation’. Maana hapa mwaka mzima mboga zitakuwa zinalimwa Nanenane. Na mabwana shamba wanapangiwa hapa kama kituo cha kazi. Hilo nahitaji litekelezwe. Mwakani kila Halmashauri itakuwa na bustani nzuri. Vilevile, ni chanzo cha mapato” alisema Waziri Jafo.

Akiongelea kilimo na ufugaji wenye tija, waziri huyo aliwataka wadau wa kilimo na mifugo kutumia fursa za tafiti zinazofanyika nchini katika maeneo hayo. Alisema kuwa tafiti hizo zinalenga kuongeza tija katika mazao ya kilimo na mifugo.

Kuhusu uendelezaji wa bidhaa za ngozi, alisema kuwa sekta hiyo inapiga hatua. “Wakati wa kutembelea mabanda nimekuta viatu vya ngozi. Hakikisheni vijana wanavaa viatu vinavyozalishwa mikoa ya Dodoma na Singida” alisema waziri Jafo. Aidha, aliwashauri wananchi kujenga utamaduni wa kununua bidhaa zinazozalishwa nchini kwa lengo la kujenga soko la ndani.

Katika salamu za Mkuu wa Mkoa wa Singida, Canon Dkt. Rehema Nchimbi  alisema kuwa Mkoa wake unafanya vizuri katika sekta ya kilimo na mifugo kutokana na uwepo wa maonesho ya Nanenane.

“Nanenane ipo pia Singida kama ilivyo Dodoma kwa tafsiri ya kuleta mabadiliko kwa wananchi wetu. Nanenane imetusaidia sana Singida. Imeifanya Singida isiwe kame, masikini na ya njaa. Tumezalisha ziada ya chakula kwa miaka mitano iliyopita. Singida tunachakula cha kutosha na hatuna njaa. Singida hatuzalishi mazao yanayostahimili ukame bali yanayotumia maji kwa ufanisi” alisema Dkt Nchimbi.

Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt Binilith Mahenge alisema kuwa Rais amejenga vituo vya afya nchi nzima na kuongeza bajeti ya dawa ili wananchi wanufaike na huduma za afya. “Mheshimiwa Waziri hakuna upungufu wa dawa. Lazima kila mwananchi awe na kadi ya bima ya afya CHF iliyoboreshwa kwa shilingi 30,000 kwa kaya na inahudumia watu sita 6” alisema Dkt Mahenge. Zaidi ya hapo utalazimika kulipa gharama ili unufaike na huduma ya afya kama hutakuwa na kadi hiyo, aliongeza.

Maonesho ya 26 ya Nanenane Nzuguni Dodoma yameshirikisha makampuni 36, wajasiriamali 300 na taasisi 43.

Waziri wa OR-TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa wajasirimali wanaoonesha bidhaa zao kwenye maonesho wa Nanenane Nzuguni alipotembelea mabanda yanayoonesha bidhaa mbalimbali. Wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Singida Canon Dkt. Rehema Nchimbi.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.