• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mhe. Ndejembi ataka maeneo ya kujenga shule yatengwe kukidhi mahitaji

Imewekwa tarehe: July 13th, 2023

NAIBU  Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Deogratius Ndejembi  alisema kuna ulazima wa kutenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa shule ili kukidhi mahitaji yanayotokana na ongezeko la wanafunzi ikiwa ni pamoja na kutatua changamoto ya wanafunzi kutembea umbali mrefu.

Ndejembi alitoa wito huo akiwa mkoani Dar es Salaam, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua ujenzi wa miundombinu ya elimu inayojengwa kupitia mradi wa BOOST na SEQUIP katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

Ndejembi alisema maeneo hayo yakitengwa, kuna ulazima wa kujenga shule za ghorofa badala ya majengo ya chini ili kutatua changamoto ya kukosa viwanja vya michezo vya watoto ambavyo ni muhimu kwa ajili ya kujenga afya ya akili.

“Michezo ni muhimu kwa ajili ya afya ya akili na makuzi ya watoto hivyo ni lazima kuwepo na ushirikiano wa viongozi kuanzia ngazi ya mtaa, kata, halmashauri, wilaya na mkoa katika kuhakikisha shule zinajengwa kwenda juu ili kupata maeneo ya viwanja vya michezo,” Ndejembi alisisitiza.

Aliongeza kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kutafuta fedha kwaajili ya kuboresha elimu ya msingi na sekondari, hivyo ni lazima kuendelea kutenga maeneo ya ujenzi na kuyatumia vizuri ili yawe na tija.

Aidha, Ndejembi aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kwa kukamilisha ujenzi wa shule mpya na ukarabati wa miundombinu ya elimu, kupitia fedha za mradi wa BOOST na SEQUIP zilizopatikana kutokana na jitihada za Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amedhamiria kuendelea kuboresha miundombimu ya elimu nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Saad Mtambule alimshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za ujenzi wa miundombinu ya elimu kupitia mradi ya BOOST na SEQUIP na kuahidi kuendelea kusimamia vizuri matumizi ya fedha hizo ili ziwe manufaa kwa taifa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.