• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Magufuli Aweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Reli ya Kisasa

Imewekwa tarehe: March 14th, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli leo tarehe 14 Marchi, 2018 ameweka jiwe la msingi la kipande cha pili cha mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) kinachoanzia Morogoro hadi Makutupora Mkoani Dodoma.

Sherehe za uwekaji jiwe la msingi katika mradi huo zimefanyika katika Kijiji cha Ihumwa nje kidogo ya Mji wa Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Tulia Ackson, Mawaziri, Makatibu Wakuu, viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama, Mabalozi wa Uturuki na Uingereza hapa nchini, Wabunge, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Dodoma Profesa Davis Mwamfupe, Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Bw. Godwin Kunambi na wananchi wa Dodoma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Bw. Masanja Kadogosa amesema ujenzi wa kipande cha pili cha reli chenye urefu wa kilometa 422 utagharimu Shilingi Trilioni 4.3 na ni sehemu ya mradi mkubwa wa ujenzi wa reli ya kati wa kuanzia Dar es Salaam hadi Mwanza yenye urefu wa kilometa 1,219.

Bw. Kadogosa amesema ujenzi wa kipande cha pili utakaofanyika kwa miezi 36 utakamilika ifikapo tarehe 25 Februari, 2021 na umetanguliwa na ujenzi wa kipande cha kwanza cha kuanzia Dar es Salaam hadi Morogoro utakaokamilika Novemba 2019.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema wakati wa ujenzi wa kipande cha pili che reli ya kati ukianza, ujenzi wa kipande cha kwanza umefikia asilimia 9 na kwamba treni zitakazotumia reli hiyo zitakuwa na uwezo wa kubeba tani 10,000 za mzigo kwa wakati mmoja (sawa na malori 500 ambayo yangesafirisha mizigo kwa barabara) na itakuwa na uwezo wa kwenda kasi ya kilometa 120 kwa saa wakati treni ya abiria itakuwa na uwezo wa kwenda kwa kasi ya kilometa 160 kwa saa.

Kabla ya kumkaribisha Mhe. Rais Magufuli, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amemshukuru kwa msukumo mkubwa aliouweka katika utekelezaji wa miradi na shughuli kubwa za Serikali ikiwemo ujenzi wa reli na amewataka watanzania kuunga mkono juhudi hizo.

Katika hotuba yake Mhe. Rais Magufuli ameelezea kufurahishwa na utekelezaji wa mradi huo ambao amesema utasaidia kurahisisha na kupunguza gharama za usafirishaji wa mizigo na abiria, na pia utaokoa barabara ambazo zinaharibika kutokana na usafirishaji wa mizigo mizito kwa magari.

"Kwa kutumia reli hii mtu atasafiri kutoka Dar es Salaam hadi hapa Dodoma kwa saa 3 tu ikilinganishwa na saa 5 hadi 6 zinazotumika hivi sasa kwa gari, na pia mtu atasafiri kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa saa 9 ikilinganishwa na saa 36 anazotumia sasa kwa kutumia treni" amesema Mhe. Rais Magufuli na kuongeza kuwa reli hiyo itakuwa na uwezo wa kusafirisha tani milioni 17 za mizigo kwa mwaka ikilinganishwa na ya sasa yenye uwezo wa kusafirisha tani milioni 5 tu.

"Bila shaka hii itaongeza mapato katika bandari yetu ya Dar es Salaam na pia kuimarisha biashara hususani kati ya nchi yetu na nchi za Burundi, DRC, Rwanda na Uganda" ameongeza Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais amewataka wananchi wa Dodoma na Watanzania kwa ujumla kuchangamkia fursa zinazotolewa na mradi huu mkubwa ambao utazalisha ajira za moja kwa moja 30,000 na zisizo za moja kwa moja 600,000 pamoja na miradi mingine ya ujenzi wa barabara, bomba la mafuta la kuanzia Hoima - Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania, mradi wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji, ukarabati wa viwanja 11 vya ndege na ujenzi wa meli ya ziwa Victoria.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemtaka Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango kufuatilia utozaji wa kodi unaofanywa na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) ili kuepusha utozaji wa viwango ambavyo ni kero na amesisitiza kuwa "inatakiwa kulipa kodi isiwe kero, iwe ni heshima".

Hata hivyo Mhe. Rais Magufuli amewataka Watanzania kuendelea kulipa kodi ili fedha zinazopatikana ziendelee kugharamia miradi ya maendeleo ikiwemo kupeleka huduma muhimu za maji, elimu, afya na umeme ambapo Serikali imedhamiria ifikapo mwaka 2021 vijiji vyote nchini vipatiwe umeme.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.