• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Samia afanya ziara Uganda

Imewekwa tarehe: April 13th, 2021

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni juzi tarehe 11 Aprili, 2021 wameshuhudia utiaji waini wa mikataba ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East Africa Crude Oil Pipeline – EACOP) kati ya Serikali na kampuni za uwekezaji uliofanyika katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda.

Hafla ya utiaji saini mikataba ya mradi huo ilihudhuriwa na Mawaziri na wawakilishi wa kampuni za uwekezaji ambazo ni Total ya nchini Ufaransa na CNOCC ya China.

Waheshimiwa Marais wameshuhudia utiaji saini wa mkataba wa kwanza ambao ni wa uenyeji wa mradi kati ya Serikali ya Uganda na wawekezaji (Total na CNOCC), mkataba wa pili wa ubia ambapo Serikali ya Tanzania na Uganda zimetiliana saini na kampuni hizo (Total na CNOCC) na mkataba wa tatu wa masuala ya kikodi na usafirishaji ambapo Serikali ya Uganda imetiliana saini na kampuni hizo (Total na CNOCC).

Pamoja na kushuhudia utiaji saini wa mikataba hiyo, Waheshimiwa Marais pia walitia saini tamko la pamoja kuhusiana na utekelezaji wa mradi huo na wameagiza vipengele vilivyobaki katika utekelezaji wa mradi huo vikamilishwe haraka.

Mradi huo utahusisha ujenzi wa bomba la mafuta lenye kutumia teknolojia ya joto (heated oil pipeline) lenye urefu wa kilometa 1,445 ambapo kati yake kilometa 1,115 zinapita Tanzania. Uwekezaji katika mradi huu unatarakiwa kugharimu Dola za Kimarekani Bilioni 3.5, uzalishaji ajira takribani 10,000 wakati wa ujenzi na utasafirisha mapipa Bilioni 6.5 ya mafuta yaliyogundulika katika bonde la ziwa Albert nchini Uganda kwenda bandari ya Tanga nchini Tanzania.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Rais Samia alimshukuru Mhe. Rais Museveni kwa kuahirisha hafla ya utiaji saini wa mikataba hiyo iliyopangwa kufanyika tarehe 22 Machi, 2021 ili kupisha maombolezo ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambaye wakati wa uhai wake alitoa mchango na msukumo mkubwa katika utekelezaji wa mradi huu mkubwa duniani.

Mhe. Rais Samia alisema mradi huu utakuwa na manufaa makubwa kwa nchi zote mbili kwa kuongeza mapato ya Taifa, kuzalisha ajira, kukuza utangamano na kuinua ustawi wa jamii.

Aidha, ametoa wito kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kuendeleza jitihada za kuimarisha miundombinu ya barabara, reli, bandari na viwanja vya ndege ili kuunga mkono uwekezaji huo pamoja na uwekezaji mwingine unaolenga kuimarisha uchumi na kuboresha maisha ya watu.

Mhe. Rais Samia amemhakikishia Mhe. Rais Museveni kuwa Serikali anayoingoza itaendeleza na kukuza zaidi ushirikiano na uhusiano wake na Uganda ikiwa ni pamoja na kuanzisha maeneo mapya ya ushirikiano.

Kwa upande wake Mhe. Rais Museveni alimshukuru Mhe. Rais Samia kwa kuitikia wito wake wa kuja kushuhudia utiaji saini wa mikataba hiyo na kufanya ziara yake ya kwanza nje ya nchi tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Rais Museveni alieleza sababu za kupitisha bomba hilo nchini Tanzania kuwa ni manufaa ya kiuchumi na pia kwa Uganda kutambua mchango wa Tanzania katika kumuondoa aliyekuwa Mtawala wa Uganda Nduli Idd Amin Dada na ushirikiano mwingine kama ndugu, jirani na rafiki wa kweli.

Aliongeza kuwa kwa kutekeleza mradi huo, Uganda pia itarahisisha mpango wake wa kununua gesi kutoka nchini Tanzania.  

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suhulu Hassan akilakiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda Mhe. Sam Kutesa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebe alipowasiri nchini Uganda kwa ziara ya kikazi ya siku moja.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suhulu Hassan akimtambulisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Liberata Mulamula kwa mwenyeji wake Rais wa Uganda  Mhe. Yoweri Museveni mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Entebbe Aprili 11, 2021 kwa ziara ya siku moja.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.