• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Miaka 46 ya CCM, Madukani watoa misaada Hospitali

Imewekwa tarehe: February 4th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KATA ya Madukani jijini Dodoma imeadhimisha miaka 46 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kutembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma ‘General Hospital’ na kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa wagonjwa na wanaowauguza kwa lengo la kuwahakikishia kuwa chama hicho kipo pamoja nao.

Mwenyekiti wa CCM Kata ya Madukani, Ezekiel Mwangosi aliyasema hayo alipoongoza viongozi wa kata hiyo kutembelea wagonjwa na kutoa misaada ya vitu mbalimbali katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

Mwangosi alisema “Kamati ya Siasa ya Kata ya Madukani tulikubaliana kuwa ni vema kuwatembelea wagonjwa na kutoa pole, kuwatakia afya njema na kuwapa zawadi ya vitu mbalimbali. Miongoni mwa vitu tulivyoleta leo ni mabeseni makubwa, chupa za chai, sabuni za unga, sabuni za miche na mafuta kwa kuvitaja vichache”.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa timu yake imefanikiwa kujionea utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM katika Kata ya Madukani na kuridhika. “Tumeshuhudia jengo kubwa la kina mama na majengo mengine yanakarabatiwa. Hivyo, hata tunapokuwa mtaani tuna mambo ya kujivunia kama wana CCM kwenye utekelezaji wa Ilani. Tunashukuru kwa kazi nzuri zinazofanywa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma ambaye ni kiongozi wa Baraza la Madiwani na maamuzi mazuri yanayofanywa na Baraza la Madiwani kwa maendeleo ya Dodoma” alisema Mwangosi.

Diwani wa Kata ya Madukani, Prof. Davis Mwamfupe alisema kuwa hospitali hiyo ipo katika kata yake. “Sisi ndio tunaona maendeleo haya na uboreshaji wa huduma za afya unaofanyika. Tuna kila sababu ya kumshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha afya za wananchi wake. Tuushukuru uongozi wa hospitali kwa kutupokea katika kutimiza dhamira yetu leo” alisema Prof. Mwamfupe.

Nae Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Kata ya Madukani, Jamila Ashery alisema kuwa hospitali hiyo ina mabadiliko makubwa ya kimiundombinu na huduma. “Hospitali ya ‘General’ haikuwa hivi, ila kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM, hospitali imekuwa bora na ya rufaa na kufanya tunajivunia wana madukani” alisema Ashery.

Kwa upande wake Muuguzi Msaidizi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Najat Kayaga alisema kuwa wagonjwa wanaohudumiwa katika hospitali hiyo wanachangamoto nyingi na ujio wa viongozi hao wa CCM Kata ya Madukani umekuwa msaada mkubwa. “Siyo kila mgonjwa anayekuja ana uwezo. Hivyo, tunawaomba mzidi kutuona na wagonjwa wetu. Mtusaidie chochote kinachopatikana tukitumie kwa pamoja. Tuwasaidie ndugu zetu ili kujenga nguvu ya taifa” alisema Kayaga.

Mheshimiwa wa Kata ya Madukani Prof. Davis Mwamfupe akikabidhi baadhi ya misaada kwa mmoja wa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma wakati wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Kata ya Madukani (CCM) walipotembelea hospitali hiyo na kutoa misaada mbalimbali. 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.