• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Miaka 5 Hospitali ya Benjamin Mkapa, makubwa yashuhudiwa

Imewekwa tarehe: October 17th, 2020

HOSPITALI ya Benjamin Mkapa (BMH) tarehe 13 Oktoba, 2020 imetimiza miaka mitano tangu ilipoanza kutoa huduma za afya kwa wananchi hapa Jijini Dodoma na mikoa ya jirani.

Katika kuadhimisha miaka hiyo mitano ya huduma, Hospitali iliandaa na kutoa bure huduma mbalimbali kuanzia tarehe 12 hadi 17, Oktoba, 2020 ambapo kulitolewa huduma ya upimaji afya kwa magonjwa ya Saratani ya matiti na shingo ya kizazi, Sikio, pua na koo, kisukari, moyo na mishipa ya damu na macho.

Aidha, huduma nyinginezo zilizotolewa ni elimu ya magonjwa ya figo na uchangiaji wa damu. Huduma hizi zilizohusisha uchunguzi wa afya zilitolewa kwa wananchi wa Dodoma na mikoa ya jirani.

Ikiwa ni sehemu ya maadhimisho hayo, Mkurugenzi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika aliwalisha keki baadhi ya wateja waliofika siku ya kwanza ya wiki la maadhimisho pamoja na baadhi ya wafanyakazi  wa BMH.

Akiongea kuhusu mafanikio ya Hospitali hiyo Dkt. Chandika alisema "Mwaka 2018 kwa kushirikiana na wadau kutoka Japan pamoja  na Chuo Kikuu cha Dodoma, tulianza kupandikiza figo, mpaka sasa tumepandikiza figo kwa wagonjwa 13, wagonjwa wawili kati yao walipandikizwa figo na madaktari wazawa. Haya ni mafanikio makubwa ndani ya miaka mitano.

BMH ina mitambo ya uchunguzi wa maradhi kama ya MRI, CT-Scan, Fluoroscopy, Mammography, huduma za mionzi (X-ray), Endoscope na vifaa vingine vingi vya kisasa. Pia imekuwa ikitoa huduma za kawaida na za kibingwa kama vile magonjwa ya ndani (internal medicine), watoto (pediatrics), upasuaji, afya ya uzazi na kizazi, upasuaji wa njia ya mkojo, upasuaji wa koo, pua na masikio na kadharika

"Hospitali hii imekuwa ikifanya vizuri pia katika matibabu ya Kifua Kikuu na tumeweza kuanzisha huduma ya kutibu saratani kwa kutumia dawa, mipango iliyopo ni kuanzisha tiba kwa kutumia mionzi" alisema Dkt. Chandika.

Ikumbukwe Hospitali ya Benjamin Mkapa imeshafanya huduma za kibingwa kupitia Huduma Tembezi "Outreach" katika mikoa ya Iringa, Singida, Manyara  na kadharika ambapo walipokuwa Iringa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, madaktari hao walilazimika kuongeza siku (zaidi ya siku 5 walizopanga) za kutoa huduma kutokana na maombi ya wagonjwa.

Vile vile, Dkt. Chandika alisema kuwa hospitali hiyo ilipozinduliwa mwaka 2015 ilikuwa na watumishi 22 wakuazimwa, lakini sasa kuna watumishi 453 baada ya Serikali kutoa kibali cha kuajiri na kuhamishia watumishi kutoka sehemu nyingine, alifafanua Mkurugenzi Dkt. Chandika.

Tazama picha za baadhi ya mitambo ya uchunguzi wa magonjwa.





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.