• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mifugo marufuku Bonde la Mzakwe - Dkt. Mahenge

Imewekwa tarehe: June 7th, 2019

SERIKALI mkoani Dodoma imepiga marufuku watu kuingiza mifugo kwenye chanzo cha maji Bonde la Mzakwe na atakayebainika kuingiza mifugo hiyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge wakati wa uzinduzi wa kampeni maalumu ya usafi wa mazingira, ambapo alisema anazo taarifa kuwa wako wananchi ambao wameanza kuingiza mifugo kwenye bonde hilo.

Aliwataka wafugaji wote pamoja na wananchi kuwa eneo hilo ambalo limetengwa kwa mipaka ni la bonde la maji la Mzakwe na kuongeza kuwa ni wajibu wa kila mwananchi kukilinda chanzo hicho muhimu.

“Ni marufuku kwa watu kuingiza mifugo kwenye chanzo cha maji bonde la Mzakwe na kwa yeyote atakayebainika kuingiza mifugo hatua zitachukuliwa dhidi yake,” alisema.

Bonde la Mzakwe ndio chanzo kikuu cha maji yanayotumika katika jiji la Dodoma na viunga vyake.

Hata hivyo, akizindua kampeni hiyo ya usafi, Mkuu huyo wa Mkoa alifurahishwa pia na Halmashauri ya Jiji kutokana na kusimamia vyema suala zima la usafi katika masoko. Pia kwa kuhamasisha uwekaji wa bidhaa kwenye meza maalumu kwa kuzingatia maelekezo ya kiafya.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo, Ofisa Masoko wa Jiji la Dodoma, James Yuna alisema mafanikio hayo yanatokana na kuendelea kuweka jitihada kubwa za usafi katika masoko yote.

Aidha mafanikio hayo pia yamechangia kuwafanya wafanyabiashara kukidhi maelekezo ya kiafya na kuepukana na magonjwa ya mlipuko yanayosababishwa na uchafuzi wa mazingira.

Ofisa huyo alisema Halmashauri ya Jiji itaendelea kuunga mkono juhudi za mkuu huyo wa mkoa za kufanya usafi mita tano kwenye maeneo ya makazi na biashara ili kuendelea kuweka mazingira mazuri.

Aidha alisema Jiji litaendelea kutoa mwito kwa wafanyabiashara wadogo maarufu machinga kufanya biashara zao kwa kuzingatia maagizo na maelekezo ya halmashauri.

Alisema maeneo hayo ni pamoja na kandokando ya barabara ili kuepusha ajali na usumbufu kwa waenda kwa miguu, kwa kuwa itatoa uhuru mkubwa kwa makundi ya watu kutumia barabara zilizopo ndani ya jiji ambao wamekuwa wakiweka pembezoni na kuathiri matumizi husika.

Mkuu wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Takangumu jijini Dodoma Dickson Kimaro, alisema kuwa kwa sasa Jiji la Dodoma wamekuwa wakipokea tani 150 mpaka 180 za taka kila siku kwenye dampo la Chidaya, jiji likishirikiana na wadau kufanikisha usafi wa mazingira.

Chanzo: Tovuti ya Habarileo (www.habarileo.co.tz)


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.