• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mifuko mbadala yawakomboa wajasiriamali

Imewekwa tarehe: July 14th, 2020

Vikundi mbalimbali vya kijamii vikiwemo vya akina Mama na Vijana vimetoa shukrani zao za dhati kwa Mfuko wa Dunia wa Hifadhi ya Wanyama pori Tanzania (WWF) pamoja na Vodacom Foundation kwa mafunzo waliyowahi kuyatoa kwa vikundi hivyo, juu ya utengenezaji wa mifuko mbadala, kwani yamezaa matunda na kuwawezesha kujiajiri, kujitegemea na kujiongezea kipato.

Hayo yamesemwa na viongozi wa vikundi hivyo katika maeneo tofauti, walipotembelewa na walezi wa vikundi hivyo kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais, waliokuwa na jukumu la kufuatilia kwa karibu vikundi hivyo ili kujua maendeleo yao.

Mwenyekiti wa kikundi cha Walengwa, ambacho kinaundwa na wanafunzi kutoka Chuo cha Serikari za Mitaa Hombolo, Baraka Peter amesema kuwa kutokana na mafunzo hayo wameweza kutengeneza na kuzalisha idadi kubwa ya mifuko ya karatasi na kuiuza, hivyo wamekua wakipata faida kubwa ambayo imewawezesha wao kama wanafunzi kujilipia ada ya Chuo na mahitaji mengine ya kiuchumi tofauti na hapo awali ambapo walikua wakiwategemea wazazi pekee.

“Miongoni mwa manufaa tuliyoyapata kutokana na mafunzo yaliyofadhiliwa na WWF pamoja na Vodacom Foundation ni pamoja na kujikwamua kiuchumi, kwasababu tukishauza mifuko hii faida tunayopata tunagawana, kingine tumekua tukipata watu ambao wamekua wakihitaji kujifunza juu ya utengenezaji wa mifuko hii kutoka kwetu hivyo tumekua tukiwafundisha na wamekua mabalozi wazuri kitu ambacho kwa upande wetu imekua ni faida mojawapo pia” – alisema Baraka Peter.

Kwa upande wake Husein Hamis ambae ni kiongozi wa Kikundi cha Kishoka kilichopo Mtaa wa Chang’ombe Jijini Dodoma amesema kuwa mwanzoni walikua wakitengeneza mifuko mbadala na ilikua ikiwaingizia kipato lakini baada ya kuona kuwa kumekua na changamoto ya mifuko hiyo kuchanika na kutoosheka baada ya kuchafuka kwa kubebea vitu kama nyama na kadharika waliamua kujiongeza na kuanza kutengeneza vikapu ambavyo ndivyo vimekua vikihitajika sana kutokana na ukubwa na uwezo wa kubebea vitu tofauti kwa wakati mmoja kwa kuwa havichaniki kiurahisi, lakini pia vimekua vikiosheka na unaweza kuvitumia zaidi ya miaka mitano bila kuchaa.

Husein aliongeza kuwa licha ya uimara wa vikapu hivyo, pia vimewaongezea kipato kwani vinauzwa kwa bei nzuri zaidi ukilinganisha na mifuko mbadala ambapo vimekua vikiuzwa kwa shilingi elfu tatu, na mtu mmoja anauwezo wa kutengeneza vikapu kumi kwa siku, hali inayopelekea kuingiza Shilingi laki tisa ndani ya Mwezi mmoja kwa kila mwanakikundi.

“Tunawashukuru sana WWF, Vodacom Foundation, Halmashauri ya Jiji letu la Dodoma pamoja na Ofisi ya Mkamu wa Rais kwa mafunzo mazuri kwani kwa upande wangu, miongoni mwa faida ninayoipata kutokana na utengenezaji wa vifungashio mbadala ni kusomesha, nina mtoto anaesoma Kidato cha Sita hivyo nimekua na uwezo wa kumlipia ada pamoja na mahitaji mengine ya shule na familia yangu kiujumla” Alisema Husein Khamis.

Nae kiongozi wa kikundi cha Faraja ambacho kinaundwa na wanawake, Bi. Asha Bahoza amesema wao ni wanufaika wakubwa wa mafunzo hayo ambapo katika hali ya tofauti wanatengeneza mifuko ya Karatasi ambayo haipitishi maji.

Asha anasema baada ya kupata malalamiko ya vifungashio vya karatasi kuchanika baada ya kuloa au kubebea mizigo mizito waliamua kutafuta njia mbadala na kupata karatasi ambazo hazipitishi maji hivyo kutatua tatizo hilo na ubora wa bidhaa zao kupanda.

Akizungumzia mafaniko waliyoyapata wao kama kikundi alisema kwanza wamekuwa wakiaminika na kupata wateja wengi kutokana na ubora wa mifuko mbadala wanayoitengeneza, lakini pia wameondoa dhana ya kuwa tegemezi katika familia zao na jamii kwa ujumla kwani wamekuwa wakiendesha maisha yao na wengine kusomesha hali ambayo hawakuwa nayo hapo awali.

Changamoto kubwa iliyoelezwa na vikundi vingi isipokua kikundi cha Kishoka ni upatikanaji wa malighafi za kutengenezea mifuko hiyo mfano gundi ambayo walielekezwa kuitumia katika mafunzo kutopatikana kirahisi na kuwalazimu kutumia gundi ya maji ambayo imekua na ufanisi mdogo.

Aidha wamewaomba wafadhili ambao ni WWF na Vodacom Foundation kuongeza mafunzo zaidi ya utengenezaji wa bidhaa nyingine lakini pia kuwapatia mitaji ya kuanzia mara baada ya kumaliza mafunzo ili iwe rahisi kwao kupata bidhaa na kuyafanyia kazi yale wanayoyapata kwenye mafunzo.

Mwenyekiti wa Kikundi cha Walengwa Baraka Peter (kulia) akiwa pamoja na wanakikundi wenzake kiwandani kwao.


Wanakikundi wakiwa wakionesha jinsi ya kutengeza mifuko mbadala mbele mwakilishi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais.


Mwenyekiti wa Kikundi cha Kishoka Hussein Hamis akitengeneza kikapu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.