• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mifuko ya Elimu kwenye halmashauri ifanye kazi kwa vitendo- Rc Senyamule

Imewekwa tarehe: May 2nd, 2024

WITO umetolewa kwa kila Wilaya za Mkoa wa Dodoma kuhakikisha mifuko ya Elimu iliyoanzishwa na Halmashauri kwa lengo la kusaidia wanafunzi wenye uhitaji inafanya kazi kwa vitendo ili kuleta tija kwa wanafunzi wanufaika na jamii kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alipokua Mgeni rasmi kwenye Hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri kwenye mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi katika shule ya Msingi Bahi Misheni iliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Bahi.

"Nitoe agizo kwa kila Wilaya zihakikishe Mifuko ya Elimu inafanya kazi kwa vitendo kama inavyofanya Bahi. Bahi mumeweka Elimu kwenye vitendo. Miaka 10 ijayo, Bahi itakua na wasomi wengi na maendeleo makubwa. Hii inadhihirisha mumemtafsiri Rais kwa vitendo" Amesema Mhe. Senyamule.

Kadhalika, Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Gifty Msuya amesema kuwa wanatarajia kuutangaza mfuko wa Elimu Bahi ufike mbali zaidi na sio kuishia Bahi tu Bali hata nje ya nchi. Pia ameongeza kuwa Wilaya yake inakwenda kuvunja rekodi na kuiheshimisha Dodoma kitaaluma.

Hata hivyo, Mkurungenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Zainab Mlawa, amesema Halmashauri yake imeshika nafasi ya 3 kwenye matokeo ya darasa la 7 mwaka jana (2023) na hafla hii ni utaratibu wa kila mwaka kutoa tuzo kwa walimu na wanafunzi waliofanya vizuri ili kutoa hamasa zaidi na shule ya Bahi Misheni ndio ilikua ya kwanza kiwilaya.

Naye Mbunge wa Bahi Mhe. Kenneth Nollo, ametoa nasaha zake kwa kuitaka jamii kushirikiana kwa karibu kwenye suala la Elimu kwani Elimu ni ya jamii yote. Amesema ni lazima kuwe na jamii iliyoelimika, yenye maendeleo na inayoendelea kujifunza kila uchao na jambo hili liwekwe katika Mkakati.

Halmashauri ya Wilaya ya Bahi ina jumla ya Shule za Msingi 86 zenye jumla ya wanafunzi 58,737 (Wav. 28,327 na Was. 30,410).

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.