• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wasiorudisha Mikopo kufikishwa Mahakamani

Imewekwa tarehe: November 2nd, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

SERIKALI ya Mkoa wa Dodoma imevitaka vikundi vinavyokopeshwa mikopo ya asilimia 10 ya fedha za mapato ya ndani na kukaidi kurudisha mikopo hiyo kufikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake ili marejesho hayo yaweze kunufaisha wananchi wengi zaidi.

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akihutubia katika hafla ya kukabidhi mfano wa hundi ya shilingi 1,389,552,700 kwa vikundi 102 vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma tukio lililofanyika katika bustani ya mapumziko ya Chinangali katikati ya Jiji la Dodoma.

Senyamule alisema kuwa fedha hizi zinazokopeshwa ni nyingi, changamoto ni kiwango cha urejeshaji. “Fedha hizi kila mtu aziheshimu na kuzitumia kwa mujibu wa malengo yaliyokusudiwa. Sheria inaruhusu mtu ambae hajarudisha mkopo kushitakiwa mahakamani. Tukaze kidogo ili watu wajue fedha hii si ya kuchezea. Wasiolipa washitakiwe mahakamani ili haki itendeke. Ndugu zangu fedha hizi siyo zawadi ni mkopo, dawa ya mkopo ni kulipa” alisema Senyamule.

Mkuu huyo wa mkoa aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kutekeleza sheria. “Pongezi kwa kutoa fedha nyingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Bado zipo halmashauri nyingi hazitoa fedha kwa mujibu wa sheria. Hii ni dhamira ya watu makini ndiyo maana fedha hizi zinatoka hapa Jiji la Dodoma. Nimefahamishwa kuwa mmepewa mafunzo ya kutosha ya mikopo hii isiyo na riba wala masharti. Sharti lililopo ni moja tu, wewe kufanya marejesho, timizeni wajibu wenu” alisema Senyamule.

Aidha, aliziagiza halmashauri za Mkoa wa Dodoma ambazo hazijatoa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani kutoa mikopo hiyo kwa mujibu wa sheria. Alisema kuwa dhamira ya serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuwawezesha wananchi wasio na uwezo wa kukopa katika taasisi za kifedha wapate fursa ya kukopeshwa.

Akiwasilisha taarifa ya utoaji mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika kipindi cha Julai-Septemba, 2022 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alisema kuwa jumla ya shilingi 1,389,552,700 zimekopeshwa wa vikundi. “Baada ya uchambuzi, jumla ya vikundi 102 viliidhinishwa kupewa mikopo yenye thamani ya shilingi 1,389,552,700 ambapo vikundi 46 vya wanawake vimekopeshwa shilingi 501,000,000, vikundi 33 vya vijana vimekopeshwa shilingi 693,294,100 na vikundi 23 vya watu wenye ulemavu vimekopeshwa shilingi 195,258,600” alisema Mkurugenzi Mafuru.

Kwa upande wa Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Jamal Ngalya alimtaja Mkuu wa Mkoa kuwa wa kwanza nchini kukabidhi kiwango kikubwa cha fedha za mikopo ya mapato ya ndani ya halmashauri. Aliwataka vijana kutumia mikopo hiyo kwa mujibu wa malengo yaliyokusudiwa. “Kwa vijana tunawaamini, tunawapa fedha za kutosha naomba msituangushe. Hivyohivyo, kina mama sijawataja sana kwa sababu sina mashaka na nyie. Mwakani tukiwa madarakani tutaomba mara mbili ya hizi fedha” alisema Ngalya.

Naye Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Dodoma, Fatma Tawfiq alisema kuwa mikopo hiyo inawasaidia sana wananchi. “Niwapongeze sana Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kutoa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani. Naamini wote hawa ni waaminifu na watarejesha mikopo hii. Pongezi kwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kazi nzuri unayoifanya na sisi bungeni tunalitambua hili na tuna kila sababu ya kukupongeza na kukutakia heri” alisema Tawfiq.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.