• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mikopo kwa vijana yatoa matunda, UVCCM yaridhishwa

Imewekwa tarehe: March 16th, 2020

MWENYEKITI wa Jumuiya ya umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dodoma, Billy Chidabwa ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuwawezesha vijana kupitia  asilimia nne ya mapato yake ya ndani inayotolewa  kwa ajili ya mikopo kwa kundi hilo.

Alisema hayo katika ziara iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita kwa lengo la  kukagua utekelezaji wa ilani juu ya asilimia nne ambapo walitembelea vikundi vitatu vya vijana ambao wanafanya ujasiriamali waliowezeshwa kwa mikopo ya Halmashauri na kuendeleza huku wakiwapatia ajira na vijana wengine ambao wako mitaani.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang'anya aliiongoza kamati ya utekelezaji ya Mkoa wa Dodoma katika miradi mitatu inayosimamiwa na vijana jijini hapo ikiwa ni pamoja na miradi wa utengenezaji wa majiko, kilimo cha kisasa cha nyanya pamoja na mgahawa wa chakula na vinywaji ambavyo vyote vinasimamiwa na vijana wabunifu waliowezeshwa  kwa kupewa mkopo na Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

"Vijana ni nguvu kazi ya taifa la sasa na lijalo, naipongeza Halmashauri ya Jiji hili hasa Mkurugenzi ambaye ni msimamizi na kiongozi kijana Godwin Kunambi kwa kujali vijana na kuwawezesha katika kuwa imara kiuchumi, vijana wengi wana ndoto kubwa lakini wanakwama kutokana na kukosa mitaji ya kuonesha walichonacho.

"Nimejionea miradi mingi na mizuri, badala ya vijana kuilalamikia Serikali kuhusu masuala ya ajira wao wamekuwa wa kwanza kutengeneza ajira kwa wenzao, mfano mzuri ni kikundi cha Youth Enterpreneurship ambao ni wadogo sana lakini wanachokifanya ni kikubwa na wanasaidia na watu wengine kujipatia kipato kwa kuwasambazia majiko wanayotengeneza", alisema Chidabwa.

Aidha, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji alieleza namna ambavyo vijana wamekuwa wathubutu ambapo kati ya vikundi vitatu vilivyotembelewa na kamati hiyo ni vijana wahitimu wa shahada katika fani tofauti walioungana na kuendeleza ujasiriamali kwa upande wa huduma ya vyakula na vinywaji, ambao mbali na ujasiriamali huo wapo na wazo ambalo wanalifanyia kazi katika kuwawezesha vijana wenzao.

"Vijana wakipewa nafasi wana vitu vingi vya kuweza kufanya, mfano hawa wa wajasiriamali wanauza chakula, Tanzania Wazalendo Youth Group wamekuja na mpango kazi wa vijana wengine, lakini wameniletea wazo ambalo kwa akili ya kawaida huwezi kulifikiria, wanatarajia kufanya kongamano la uhamasishaji kwa vijana wenzao, linaloitwa "Great Minds Event"  hivyo tujitahidi kuwasapoti kwa kadri tutakavyojaliwa, waweze kufanikisha ndoto walizonazo", alisema Nabalang'anya.

Ziara hiyo ilihusisha jumuiya ya siasa ya vijana Mkoa, walifika na kujionea shughuli zinazofanywa na vijana wathubutu, ambao wamewezeshwa kwa kupatiwa mikopo na Halmashauri ili kuweza kuendeleza ujuzi walionao katika maeneo yao ya kazi, ikiwa ni katika kikundi cha Wanana, Youth Enterpreneurship, pamoja na Tanzania Wazalendo Youth Group.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.