• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mikopo ya asilimia 10 yawang’arisha wajasiriamali Makutupora

Imewekwa tarehe: April 16th, 2025

Na. Nancy Kivuyo, MAKUTUPORA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupitia utoaji wa mikopo ya asilimia 10 yanufaisha makundi ya wanawake katika kujikwamua kiuchumi katika Kata ya Makutupora ikitajwa kuwa chachu ya kuinua maendeleo katika sekta ya kilimo, ufugaji na ujasiriamali.

Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na makundi ya wanawake waliopata mikopo ya asilimia 10 katika Kata ya Makutupora, Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Makutupora, Andrew Boma alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kusimamia vema uwezeshaji wa wananchi kupata haki zao hasa kwa makundi maalum ambayo yamewezeshwa kupitia mikopo hiyo. “Sisi Kata ya Makutupora vikundi 20 vimepatiwa mkopo wa jumla ya shilingi 230,000,000. Vikundi vya wanawake ni 10, vijana saba na watu wenye ulemavu vitatu. Mpaka sasa wameweza kurejesha shilingi 159, 980,000 na bakaa inaendelea kulipwa na vikundi hivyo” alisema Boma. 

Aliongeza kuwa vikundi hivyo vinajishughulisha na shughuli mbalimbali kama useremala, ushonaji, ufundi ‘welding’ na biashara ya bodaboda ambazo zinawawezesha kuongeza kipato na kumudu gharama za maisha. “Kimsingi tunamshukuru sana rais wetu kwasababu ameweza kugusa maisha ya watu wenye uhitaji. Mikopo hii imesaidia wananchi kuongeza kipato, kununua mahitaji ya watoto, kununua mali kama viwanja, kumudu gharama za matibabu na kuendesha maisha yao. Kiujumla serikali, mheshimiwa mbunge na diwani nao wana mchango mkubwa sana kwasababu wamekuwa wakitusemea huko kwenye vikao na kufanya umoja wao kuwa na mabadiliko chanya kwa jamii ya Makutupora” aliongeza Boma.

Alisema kuwa anawajibu wa kuhakikisha shughuli za maendeleo katika kata hiyo zinakuwa na mafanikio kupitia elimu na uhamasishaji. “Kiukweli maendeleo ya jamii ni muhimu katika kuboresha maisha ya wananchi kwa ujumla. Mimi hapa Kata ya Makutupora hakuna eneo naweza kulikwepa, kwasababu mambo yote ya msingi yanayomgusa na kumjenga mwananchi nayahudumia kwa kushirikiana na watalaam wengine” alieleza Boma.

Nae, Afisa Mtendaji wa Kata ya Makutupora, Hamisi Jigwa alisema kuwa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa mkombozi kwa wananchi wa Makutupora. “Tunaipongeza sana serikali kupitia rais wetu mpendwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuyajali makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Kupitia mikopo hiyo, wanavikundi wamepata faida ambayo inawasaidia kulipa ada za watoto, kununua mahitaji na wengine wamefikia hatua ya kuanzisha miradi mingine iliyotokana na faida. Kwahiyo, niwaase watu wenye uhitaji wa mikopo watembelee ofisi za kata watapata maelekezo namna mikopo hiyo inavyopatikana” alisema Jigwa.  



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.