• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Milango ya uwekezaji Dodoma yafunguliwa kwa wakazi wa Geita

Imewekwa tarehe: December 2nd, 2020

Watumishi mkoani Geita wameshauriwa kuchangamkia fursa za uwekezaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ili kujenga na kukuza uchumi wao na taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo ilitolewa na kaimu Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Utawala na Rasilimali watu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ally Mketo alipokuwa akifungua kikao baina ya watumishi wa Mkoa wa Geita na wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma waliotembelea Mkoa huo kuelezea fursa za uwekezaji zinazopatikana Dodoma katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Mketo alisema “timu ya wataalam kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma karibuni sana Mkoa wa Geita, mpo sehemu salama. Watumishi wa Mkoa wa Geita wana ari ya kufahamu Jiji la Dodoma lina fursa gani ili waweze kunufaika nazo”. Alisema kuwa fursa zinapatikana kwa nadra, na kuwashauri kutumia nafasi hiyo kwa manufaa ya uwekezaji na kukuza kipato chao na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake, Afisa Menejimenti Fedha katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, Felix Mabula alisema kuwa fursa za uwekezaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni jambo la msingi ambalo linatakiwa kuwanufaisha watanzania wote. “Fursa za viwanja mara nyingi unapokuwa kijana unahisi hazikuhusu, umri unaposogea ukija kutahamaki unajikuta umechelewa na kuanza kulalamika” alisema Mabula.

Akiwasilisha mada juu ya mipango na fursa za uwekezaji zinazopatikana katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mchumi katika Halmashauri hiyo, Fred Robert alisema kuwa fursa za uwekezaji haziwatengi watumishi wa umma na wawekezaji wengine. “Uwekezaji ni uendeshaji wa uchumi, hivyo kila mtu ana haki sawa katika kuchangamkia fursa za uwekezaji katika Jiji la Dodoma” alisema Robert.

Akiongelea fursa zilizoainishwa kutoka katika Mpango Kabambe wa Halmashauri hiyo, Robert alizitaja kuwa ni uwekezaji katika maeneo ya elimu, afya, biashara, kilimo na burudani. “Fursa zipo katika uwekezaji wa ujenzi wa vyuo na shule. Maeneo menginge ni ujenzi wa hospitali, vituo vya afya na zahanati” alisema Robert.

Akiongelea fursa za uwekezaji katika biashara, alizitaja kuwa ni uwekezaji katika ujenzi wa viwanda, hoteli, na maduka makubwa. “Halmashauri pia imetenga maeneo kwa ajili ya kilimo cha Kisasa na maeneo ya kuweka ranchi” alisema Robert.

Akiongelea urahisi wa kuwekeza katika Jiji la Dodoma, Robert alisema kuwa Jiji hilo lina maeneo yaliyopangwa na miundombinu iliyosanifiwa vizuri na hakuna msongamano wa magari kutokana na kuwepo kwa mpangilio mzuri wa mfumo wa barabara. “Gharama za kutwaa ardhi ni nafuu na ni rahisi kupata hati milki za ardhi kutoka Halmashauri ya Jiji na kuna wepesi katika kuidhinishiwa ramani na vibali vya ujenzi” alisema.

Nyingine ni uwepo wa rasilimali ardhi ya kutosha na hali ya hewa nzuri. Jiji hilo lipo katika eneo la kimkakati kwa uwekezaji likifikika kirahisi na kupitiwa na barabara kuu (the Great North) inayounganisha miji ya Johannesburg (Afrika Kusini) na Cairo (Misri).



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.