• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Milioni 235.9 zatolewa ukarabati wa jengo la Zahanati ya Ihumwa

Imewekwa tarehe: October 23rd, 2023

Wahisani kutoka Shirika la ABBOT wametoa kiasi cha shilingi milioni 235.9 kwaajili ya ukarabati wa jengo la Zahanati ya Ihumwa, lengo likiwa kuboresha huduma za afya hasa huduma za dharura ambazo zinaenda kupunguza vifo vya wagonjwa mahututi/ majeruhi katika kata hiyo.

Hayo aliyasema Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Dkt. Andrew Method alipokuwa akisoma taarifa ya mradi mbele ya Kamati ya Fedha na Utawala walipofanya ziara ya kukagua mradi huo.

Dkt. Method alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutasaidia zaidi ya wakazi 24112 wa Kata ya Ihumwa na kata jirani pia utapunguza idadi ya vifo vinavyotokana na wagonjwa mahututi kwa kusogeza huduma za dharura karibu zaidi na wananchi.

“Tunashukuru Shirika la Wahisani ABBOT kwa kutoa fedha kwaajili ya kuimarisha miundombinu ya afya katika Zahanati ya Ihumwa. Serikali na washirika wake baada ya kuona huduma za dharura katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbli na zimeonesha matokeo chanya katika kuokoa maisha, ikaona ni busara huduma hii kuanzishwa kwenye ngazi ya zahanati. Katika awamu hii zahanati mbili na kituo cha afya kimoja zinatarajia kuanzisha huduma hii hivyo, kuifanya Zahanati ya ihumwa kuwa moja kati ya zahanati zitakazotoa huduma ya dharura” alisema Dkt. Method.

Kwaupande wake Diwani Neema Mwaluko, Mjumbe kutoka Kamati ya Fedha na Utawala alilipongeza Shirika la ABBOT kwa fedha walizotoa kwaajili ya ukarabati wa zahanati hiyo na kuiomba Kamati ya Fedha na Utawala iridhie kupokea changamoto zilizosomwa kwenye taarifa na kuzifanyia kazi.

“Daktari ametwambia ujenzi huu hautahusisha ujenzi wa uzio, ujenzi wa vyoo vya nje wala uwekaji wa vigae vya chini. Wenzetu wametusaidia nasisi tunatakiwa kuweka mkono kuhakikisha zahanati hii inakamilika kwa ubora unaotakiwa, hii zahanati ni yakwetu inaenda kuhudumia wananchi wetu tusimamie kwa ukaribu kuhakikisha changamoto zinatatuliwa” alisema Diwani Mwaluko.

Naye Diwani Elis Kitendya, Mjumbe kutoka Kamati ya Fedha na Utawala alishauri kujengwe kisima kwenye eneo la mradi sababu miradi mingi inakamilika ila maji yamekuwa ni changamoto kubwa. “Zahanati hii inakwenda kuhudumia maelfu ya wananchi bila kuwa na maji ya uhakika tutajikuta tunazalisha magonjwa mengine ya mlipuko. Tuhakikishe tunaweka miundombinu  ya maji sawa hasa kuchimba kisima ili kutatua shida ya maji” alimalizia Kitendya.

Mradi wa Ukarabati wa Jengo la Zahanati ya Ihumwa ulianza tarehe 10/08/2023 unatarajiwa kukamilika tarehe 28/12/2023, ukigharimu kiasi cha shilingi milioni 235.9 fedha kutoka Shirika la Wahisani ABBOT.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.