• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Milioni 544,225,626 zatolewa kujenga shule mpya ya sekondari Michese

Imewekwa tarehe: March 26th, 2024

Na. Dennis Gondwe, MKONZE

RAIS, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha shilingi 544,225,626 kujenga Shule mpya ya Sekondari Michese ili kupunguza msongamano katika Shule ya Sekondari Mkonze na kuwapunguzia wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya elimu.

Kauli hiyo ilitolewa na mwakilishi wa Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Fredrick Mwakisambwe alipoongoza waandishi wa habari kutembelea Shule mpya ya Sekondari Michese iliyojengwa katika Kata ya Mkonze jijini Dodoma.

Mwl. Mwakisambwe ambae ni Afisa Elimu Vifaa na Takwimu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema “ndugu waandishi wa habari, tupo Kata ya Mkonze eneo la Michese. Eneo hili ni moja ya maeneo yaliyonufaika na kujengwa shule mpya ya sekondari. Kata ya Mkonze ina idadi kubwa ya wananchi na kwa muda mrefu ilikuwa na shule moja ya sekondari ya kata. Mwaka huu 2024 idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza katika kata ilikua ni wanafunzi 700. Idadi hiyo ni kubwa kuhudumiwa kwenye shule moja ya Sekondari Mkonze. Hivyo, serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweza kutuletea fedha shilingi 544,225,626 kujenga majengo haya yanayoonekana mazuri na ya kisasa. Madarasa nane, Maabara tatu, jengo la maktaba, jengo la Tehama, jengo la utawala na matundu ya vyoo”.

Alisema kuwa shule hiyo itasaidia mazingira bora ya kujifunzia kwa wanafunzi na kufundishia kwa walimu. “Kwa kipekee kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na halmashauri tunashukuru sana juhudi hizi na watoto watasoma katika shule hii kwa umbali usio mrefu sana. Tunaipongeza sana serikali kwa uwekezaji huu mkubwa. Na sisi tunaahidi kusimamia taaluma katika Jiji la Dodoma ili juhudi hizi tusimuangushe mheshimiwa Rais” alisema Mwl. Mwakisambwe kwa kujiamini.

Msimamizi wa ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Michese, ambae ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Mkonze, Mwl. Andrew Rumishael alisema kuwa Kata ya Mkonze ni kubwa ilihitaji shule mpya muda mrefu kwa sababu iliyopo ilizidiwa wingi wa wanafunzi. “Kulikuwa na idadi kubwa sana ya wanafunzi wanaoishi Michese waliokuwa wakitembelea kuifuata Shule ya Sekondari Mkonze. Shule hii itapunguza umbali wa karibu kilomita nane walizokuwa wakitembea wanafunzi kwenda na kurudi na kufanya wawe na nguvu ya kutulia na kusoma vizuri na hata ufaulu wao utaongezeka kwa sababu ya kupunguza umbali huo wa kutembea” alisema Mwl. Rumishael.

Aliongeza kuwa shule hiyo itasaidia kumlinda mtoto wa kike kumaliza masomo yake dhidi ya changamoto za mimba. “Shule hii itamsaidia mtoto wa kike kuzingatia masomo yake na kufikia malengo yake. Tunaishukuru sana serikali ya awamu ya sita kwa kujali elimu na kumlinda mtoto wa kike na kuhakikisha anatimiza malengo yake” alisema Mwl. Rumishael.

Kwa upande wa mkazi wa Michese Isaya Halwa alipongeza maono ya Rais ya kuboresha mazingira ya elimu kwa watoto katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Hapo awali watoto wetu walikuwa wanasoma mbali na na elimu ilikuwa shida sana. Tunamshukuru Mungu sababu ya maono na kujituma kwake kuanngalia mazingira ya wananchi wanachohitaji. Mheshimiwa Rais ameona aanze kuandaa kizazi bora cha kesho, sasa tunaona mwanga ambao hatukuwa tukiuona hapo awali” alimalizia Halwa.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.