• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Miundombinu S/M Uhuru chachu ya elimu bora

Imewekwa tarehe: May 17th, 2025

Na. Aisha Ibrahim, UHURU

Diwani wa Kata ya Uhuru, Halfan Kabwe, ameishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya utawala wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi kubwa ya kukuza sekta ya elimu kwa maendeleo ya Jiji la Dodoma na taifa kwa ujumla.

Alitoa shukrani hizo wakati akitoa ufafanuzi wa pesa alizopokea katika kata yake kwaajili ya kukamilisha ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi Uhuru, uliogharimu shilingi milioni 76. 

Akitoa ufafanuzi wa kina kuhusu ukamilifu wa vyumba vya madarasa alisema, “kupitia serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alitupatia kiasi cha shilingi milioni 50 ambazo tuliweza kujenga madarasa 10 na baadae akatuongeza kiasi cha shilingi milioni 26 zilizotuwezesha kukamilisha ujenzi wa madarasa hayo” alisema Diwani Kabwe.

Katika hatua nyingine, alimpongeza mbunge kwa kuwa na moyo wa kujitolea kufuatia ujenzi wa uzio katika shule hiyo kwalengo la kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora kupitia mazingira rafiki. “Nichukue fursa hii kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Mheshimiwa Anthony Mavunde, kwa kutusaidia kujenga uzio wa shule hii kwa kutumia fedha zake mwenyewe ambapo kabla ya hapo kulikuwa na changamoto kwa wanafunzi kwasababu sehemu kubwa ya shule hii ilikuwa imevamiwa na magari ya mizigo” alisema.

Pia, aliahidi kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya elimu ikiwemo kutunza miundombinu ya shule hiyo na kupandisha ufaulu wa wanafunzi kwa maendeleo ya taifa kwa ujumla. “Tunaahidi kufanya makubwa katika sekta ya elimu ikiwemo kutunza miundombinu ya shule hii na kuhakikisha wanafunzi wanafaulu kwa kiwango cha juu kwasababu Dkt. Samia Suluhu Hassan anatudai deni kubwa sana kupitia uwekezaji huu” aliongeza Diwani Kabwe.

Kwa upande wake, Mwl. Sospeter Ramadhan, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru, alieleza kuwa kabla ya kujengwa kwa uzio wa shule hiyo kulikuwa na changamoto kwa wanafunzi katika suala ya nidhamu na taaluma. Sababu kubwa mazingira hayo yamezungukwa na wafanyabiashara wengi waliokuwa wanasababisha muingiliano na wanafunzi jambo linalopelekea washindwe kujifunza kwa utulivu. 

Sambamba na hayo, mwanafunzi kutoka shule ya Msingi Uhuru, Fathiya Saleh, alieleza kuwa kabla ya kujengwa uzio walikuwa wanakutana na vishawishi mbalimbali kutoka kwa wafanyabiashara wa eneo hilo. Pia vitisho kutoka kwa  walevi na vichaa wanaoingia eneo la shule jambo lililokuwa linapelekea kukosa amani wawapo shuleni hasa kipindi cha mapumziko.

Nae, Ikram Mohamed, mwanafunzi kutoka shule hiyo, aliishukuru serikali kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa na uzio kwasababu kabla ya hapo walikuwa wanashindwa kukaa darasani na kusoma kwa utulivu. Pia aliahidi kusoma kwa bidii ili kuunga juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma atoa pongezi kwa Madiwani

    May 25, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Wananchi Kata ya Madukani washukuru kuboreshwa huduma za Afya, Zahanati ya Chikande

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.