• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Miundombinu ya shule ikamilike kwa wakati - Kunambi

Imewekwa tarehe: January 4th, 2020

Wakuu wa Shule, Watendaji wa Kata na Maafisa Elimu, wametakiwa kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa Madarasa na Mahabara  katika shule zao, kabla ya tarehe ya kufungua shule kwa muhula wa masomo wa mwaka 2020.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi alipokua akizungumza na Wakuu wa Shule, Watendaji Kata na Maafisa Elimu Kata kwenye kikao kazi cha ndani cha kiutendaji kilichokua na lengo la kufanya tathmini ya ujenzi wa madarasa na mahabara katika Shule za Msingi na Sekondari Jijini Dodoma.

Kunambi amesema kuwa iwapo mpaka kufikia tarehe ya kufungua shule ujenzi huo utakua haujakamilika na pesa za kujengea zipo kwenye akaunti na zimeingizwa kwa muda mrefu, viongozi hao waandae maelezo ya kwanini waendelee kuwa katika nafasi walizo nazo.

Vilevile amewataka wakuu wa Shule kuhakikisha wanafunzi wote wanaingia madarasani na kuwafuatilia wale wote ambao hawaingii madarasani, kujua sababu zinazowapelekea kutofanya hivyo.

Kwa upande mwingine Mkuu wa Idara ya Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji wa Jiji la Dodoma Shabani Juma ameshangazwa na baadhi ya wakuu wa Shule jijini hapa, kushindwa kufanya ukarabati mdogo wa baadhi ya vitu katika shule zao kama vile viti, meza na milango licha ya mambo hayo kuwa ndani ya uwezo wao.

Shabani amewataka waalimu hao kutoishi kama wapangaji, huku akiwahimiza kuwa wabunifu na kuzipenda shule zao kutokana na baadhi ya shule kuwa na miradi inayowaingizia pesa ambazo zingewawezesha kukarabati vitu mbalimbali kama vile madawati na milango.

Nae Mkuu wa Idara ya Fedha na Biashara wa Jiji la Dodoma Alfred Mlowe amewakumbusha viongozi hao kuwa fedha zinazotumika katika ujenzi na ukarabati ni fedha za Serikali hivyo matumizi ya fedha hizo yanatakiwa yazingatie na yafuate sheria, kanuni na miongozo ya Serikali kwa sababu mwisho matumizi hayo ni lazima yakaguliwe.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi alipokuwa akiongea na waalimu wakuu wa shule za msingi na sekondari, watendaji na maafisa elimu kata (hawapo pichani) kuhimiza juu ya umaliziaji wa miundombinu ya shule za jiji kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza.


Mkuu wa Idara ya Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji Shabani Juma akiongea wakati wa kikao kazi na watendaji na maafisa elimu kata pamoja na walilmu wakuu wa shule za Jiji la Dodoma.


Mkuu wa Idara ya Fedha na Biashara wa Jiji la Dodoma Alfred Mlowe akizungumza na washiriki wa kikao kazi kilichohusu umaliziaji wa miundombinu ya shule kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza 2020.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.