• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkaguzi apongeza Jiji kwa hati safi, Mkurugenzi aonya kutobweteka

Imewekwa tarehe: June 13th, 2019

MKURUGENZI wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi amewataka viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutobweteka baada ya kupata hati safi kwenye taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha wa unaoishia Juni 2018.

Akizungumza kwenye kikao maalum cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Jiji Juni 12, Mwaka huu,  Kunambi alisema kuwa Halmashauri ya Jiji hilo imefanikiwa kupata hati safi kutokana na kujibu ipasavyo hoja zote 54 zilizotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali katika mwaka wa fedha 2017/18 na kwamba kati ya hoja hizo, 17 ni hoja za zamani na 37 ni hoja mpya.

“Kutokana na utendaji bora, usimamizi mzuri wa miradi, ukusanyaji mapato kwenye vyanzo vyetu vya ndani, Halmashauri ya Jiji la Dodoma tumeweza kujibu Hoja zote 54 ndani ya siku 21 kama inavyotakiwa kwa mujibu wa sheria, tumeweza kupunguza hoja za mkaguzi kwa kiwango cha hoja 77, ukilinganisha na hoja za mwaka wa fedha 2016/17 ambapo tulikuwa na jumla ya hoja 131”  Alisema Kunambi.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa,  kutokana na watendaji bora wa Halmashauri yake pamoja na madiwani kufanya kazi kwa ushirikiano katika suala zima la kuhakikisha mapato yanakusanywa kwa kiwango kikubwa ndiyo sababu ya kuweza kupunguza hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali kila mwaka.

‘’Nawapongeza watendaji wa Halmashauri na madiwani kwa kufanya kazi kwa ushirikiano na kufanikiwa kupata hati safi, hivyo nawaomba muongeze kasi zaidi kiutendaji na kamwe msibweteke,’’alisema Kunambi

Hata hivyo, Katika ukaguzi wa fedha wa mwaka 2017/18 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali ametoa hati safi yenye msisitizo, na kwa upande wa mifuko mbalimbali, Mdhibiti ametoa hati safi kwa mifuko yote kwa mwaka wa fedha 2017/18.

Aidha, Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo Devis Mwamfupe amesema kuwa kupatikana kwa hati safi katika Halmashauri hiyo kutachochea zaidi kasi ya utendaji kazi ili kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Mwamfupe aliwahimiza Madiwani kufanya kazi kwa ushirikiano na kuepuka kufanya kazi kwa mazoea na kuwataka kuwatendea haki wananchi ambao wamewachagua kwa kuhakikisha maendeleo yanawafikia kwa kuwatataulia kero zinazowakabili.

Kwa upande wa Mkaguzi Mkuu wa nje wa Mkoa wa Dodoma Chami Ngelela amewapongeza viongozi wa Halmashauri hiyo kwa kupata hati safi kwa mwaka wa pili mfululizo na kuendelea kuitetea hati hiyo na kupongeza ushirikiano mzuri wanaopatiwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuweza kujibu hoja zinazotolewa kwa wakati.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.