• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkoa wa Dodoma wakamilisha maandalizi uibuaji wagonjwa wenye vimelea vya Kifua kikuu

Imewekwa tarehe: January 18th, 2025

Na. Hellen M. Minja,

Habari - DODOMA RS

Ikiwa ni siku ya tatu ya mafunzo kwa Wataalam wanaotoa huduma kwa wagonjwa wa Kifua Kikuu, leo Januari 17, 2025, Mkoa wa Dodoma umekamilisha mafunzo hayo kwa Halmashauri za Kondoa Mji na Kondoa Vijijini ambayo yamefanyika kwenye ukumbi wa Kondoa Irangi, Halmashauri ya Kondoa wa Mji.

Mafunzo hayo yanalenga kukuza uelewa kuhusu namna ya kufanikisha mpango wa kuibua wagonjwa wenye vimelea vya Kifua Kikuu unaotarajiwa kuanza kutekelezwa rasmi siku ya Jumatatu, Januari 20 kwenye Halmashauri 76 za Mikoa 9 Nchini ambapo Mpango huo mahsusi ulizinduliwa na Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama mnamo Januari 06 Mkoani hapa.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo yanayoratibiwa na Serikali ya Mkoa chini ya Wizara ya Afya, Mratibu wa huduma za kudhibiti Kifua Kikuu kutoka Wizara hiyo Dkt. Allan Tarimo, amesema Mkoa wa Dodoma ndio nyenzo kuu Kati ya Mikoa 9 iliyopo kwenye Mpango kwani ndio Makao Makuu ya Nchi hivyo inabidi kuchimba zaidi ili kuwapata wagonjwa wote.

Aidha, Mratibu wa Huduma za Kifua Kikuu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Peres Lukango, amesema;

"Kondoa ina takribani wagonjwa 800 ambao hawakufikiwa mwaka jana hivyo wanatakiwa kuibuliwa wakati wa Mpango huu na tukiwa na dhamira moja, tutaweza. Leo tunamalizia mafunzo kwa Halmashauri zote 7 zilizopo kwenye Mpango, Wataalam wamendaliwa vizuri vituoni na nyenzo zote zimekamilika tayari kwa kuanza zoezi."

Kadhalika, Mshauri wa zoezi la kuibua wagonjwa wenye vimelea vya Kifua Kikuu kutoka Wizara ya Afya nchini Uganda Dr. Turyah Stavia, amehudhuria mafunzo hayo ili kutoa uzoefu wa nchi yake ambayo imefanikiwa kwenye zoezi hilo.

"Nimekuja kutoa msaada kwa Wizara ya Afya kwenye hii kampeni kwa kuwa ukitafuta wagonjwa wa Kifua Kikuu, utawapata. Tunahitaji kumaliza Kifua Kikuu ifikapo 2030 na hatuwezi bila kuwapata wagonjwa wote. Tunapaswa tujiulize nini cha kufanya ili wapatikane? Na ndio kinachofanyika hapa." Dr. Stavia.

Mkoa wa Dodoma unatarajia kuibua wagonjwa wenye vimelea vya Kifua Kikuu wapatao 1,930 ambao hawakupatikana wakati wa zoezi la mwaka 2024.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.