• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dawa ya Mkopo ni Kulipa - Senyamule

Imewekwa tarehe: November 2nd, 2022

Na. Theresia Nkwanga, DODOMA

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wanufaika wa mkopo wa asilimia 10 ya Halmshauri kuhakikisha wanarejesha fedha za mikopo kama sheria inavyowataka ili fedha hizo ziweze kuwanufaisha watanzania wengine wanaohitaji mkopo.

Wito huo ameutoa aliposhiriki tukio la utoaji Hundi ya mfano kwa  vikundi vilivyopata mkopo vya wanawake, vijana na wenye ulemavu tukio lililofanyika katika bustani ya mapumziko ya Chinangali iliyopo jijini Dodoma.

Senyamulle alisema kuwa ni wakati sasa kuhakikisha wanufaika wa mkopo wanatumia mikopo waliyopewa na Halmashauri kimkamkati, kiufanisi na kwa umakini mkubwa kwenye kujikomboa kiuchumi na kurejesha kwa wakati ili watanzania wengine waweze kufaidika.

“Matarajio ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kwamba mkikopeshwa fedha hizi mtazirejesha ili na wenzenu waweze kukopa, ningetamani kuona kila aliyepewa fedha hizi anaziheshimu, fedha hii sio zawadi ni fedha ya mkopo na dawa ya mkopo ni kulipa. Nitoe wito kwenu twende tukapeane shime, tukashikamane tukanyoosheane vidole fedha hizi tuzirudishe ili na wenzetu wapate bahati tulopata sisi na sisi tupate bahati yakukopeshwa tena kiasi kikubwa zaidi yatulichopata leo.

Nikuagize Mkurugenzi sheria inaruhusu mtu ambaye hajarudisha mkopo kushtakiwa mahakamani na kufunguliwa kesi, Hili limekua likifanyika kwa uzembe kidogo na kwa huruma sana, ni wakati sasa tuamue kukaza kidogo ili wajue kuwa fedha hii si yakuchezea pia tutawafundisha matumizi ya fedha yanataka nidhamu’’.

Akiongelea dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan, Senyamule alisema  dhamira ya Rais Samia nikuhakikisha watanzania wasio na vigezo na wasio na uwezo wa kukopa benki kwenye masharti ya kurudisha riba kubwa na masharti makubwa yakuweka dhamana, wanapata nafasi ya kufanya biashara mbalimbali kwa kukopeshwa na Halmashauri zao mikopo isiyo na riba yenye masharti nafuu yakurejesha ulichokopa tu.

Akisoma taarifa ya utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake vijana na watu wenye ulemavu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alisema  katika kipindi cha Julai hadi Septemba Halmashauri ya Jiji la Dodoma imepokea maombi kutoka vikundi 198 vya wanawake vijana na wenye ulemavu yenye thamani ya shilingi bilioni 5.8, baada ya uchambuzi yakinifu jumla vikundi 102 viliidhinishwa nakupewa mikopo yenye thamani ya sh bil 1.3 kati ya vikundi hivo wanawake ni  vikundi 46 vijana 33 na watu wenye ulemavu 23.

Naye, Asha Hamisi Mwenyekiti wa kikundi cha Paza Sauti kilichopo Changombe jijini Dodoma kikundi kinachojishughulisha na kukamua alizeti na kuuza mafuta, alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa maono yake yakuhakikisha watanzania wanafaidika na fedha zao kupitia mikopo isiyo na riba.

“Kwaniaba ya kikundi cha Paza Sauti nimshukuru Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kutupatia kiasi cha shilingi milioni tano, kupitia mkopo huu pato letu litaongezeka na mtaji wetu wa biashara unaenda kukua, tumejipanga kurejesha vizuri ili tuweze kupata kiasi kikubwa zaidi awamu ijayo tunawashauri watu walioko mtaani wajitokeze kuomba mikopo hii ni halisi’’.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.