• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkurugenzi apita nyumba kwa nyumba kutatua migogoro ya ardhi

Imewekwa tarehe: June 13th, 2019

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Godwin Kunambi amefanya ziara ya nyumba kwa nyumba kutembelea maeneo yenye migogoro ya ardhi katika Kata ya Ipagala ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu.

Kunambi amechukua hatua hiyo baada ya kugundua kuwa, idadi kubwa ya wananchi wanaofika katika Ofisi za Jiji hilo kutafuta ufumbuzi wa kero mbalimbali zinazohusu ardhi wanatoka katika Kata hiyo. 

Ziara ya Mkurugenzi huyo ililenga kukagua uvamizi wa baadhi ya maeneo uliofanywa na wananchi ikiwemo shule, vituo vya afya, viwanja vya michezo, maeneo ya wazi na hifadhi za barabara.

“Hatuwezi kukubali tukose maeneo ya zahanati, shule, au viwanja vya michezo kwa sababu ya baadhi ya watu wachache wasio waaminifu ambao wamekuwa wakimega na kuuza maeneo ya wazi” Alisema Kunambi.

“Sasa tutengeneze utaratibu wetu kwenye mitaa wa kujisimamia wenyewe katika udhibiti wa mambo yanayokwenda kinyume na utaratibu, viongozi wa mitaa kwa kushirikiana na wananchi wakemee uvutaji wa bangi na madawa ya kulevya kwa watoto, kudhibiti ujenzi holela, na kuwachukulia hatua wanaojenga kwenye hifadhi za barabara” Aliongeza Kunambi.

Naye Diwani wa Kata ya Ipagala Kamuli Gombo alisema kuwa, kwa muda wa miaka 26 sasa wananchi wamepimiwa eneo hili lakini migogoro haijawahi kuisha kwa sababu ya kuendekeza urafiki kati ya viongozi na wananchi.

“Kama kuna mtu anastahili kubaki na abaki, lakini kama kuna mtu hastahili na atoke ili suala hili liishe” Alisema Gombo

Baadhi ya Wananchi wamempongeza Mkurugenzi wa Jiji kwa kutembea nyumba kwa nyumba na mtaa kwa mtaa kwa kuwa kitendo hicho kimelenga kutatua migogoro yao iliyodumu kwa miaka mingi.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma yupo katika ziara ya mtaa kwa mtaa kwenye Kata zote zenye historia ya migogoro ya ardhi iliyodumu kwa muda mrefu kwa lengo la kumaliza kero hizo ili wananchi waendelee kujenga na kuendeleza makazi yaliyopangwa ndani ya Jiji.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.