• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkurugenzi Msaidizi Habari-MAELEZO atoa neno kwa Dodoma FC

Imewekwa tarehe: August 21st, 2019

Uongozi wa timu ya mpira wa miguu ya Dodoma FC inayomilikiwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma, umeshauriwa kutumia vyombo vya habari kuitangaza timu hiyo na kuhamasisha wananchi kuiunga mkono.  

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Msaidizi-Huduma za Habari na Picha wa Idara ya Habari-MAELEZO, kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Rodney Thadeus ofisini kwake leo, alipokuwa akiongelea umuhimu wa vyombo vya habari katika kuitangaza timu ya Dodoma FC.

Rodney alisema kuwa vyombo vya habari vina mchango mkubwa katika kuitangaza timu hiyo kwa wananchi na kuushauri uongozi wa timu hiyo kutumia vyombo mbalimbali vya habari kama redio, magazeti na mitandao ya kijamii kuhamasisha wananchi wa Dodoma.

“Watu wanataka kupata taarifa kuhusu timu yao kila mara ili wahamasike katika kuisaidia na kuishangilia pale inapokuwa na mechi. Sasa hili ni jukumu la Afisa Habari wa timu. Karibu Redio zote zina vipindi vya michezo, hivyo tengenezeni mtandao utakaowasaidia kuitangaza timu ya Dodoma FC kupitia vipindi hivyo”, alisema Rodney.

Mkurugenzi huyo Msaidizi alisema kuwa mafanikio ya timu yanategemea sana hamasa kutoka kwa wachezaji wenyewe na mashabiki wa timu hiyo na ili kufanikisha hilo, ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi timu hiyo inapocheza ili kuwapa hamasa wachezaji. “Mimi nimeishajiwekea utaratibu pale ambapo sina majukumu ya kikazi, mechi zote za Dodoma FC nitakuwa nahudhuria maana hii ndiyo timu yetu wana Dodoma na tunatakiwa tuisaidie ili iweze kupanda ligi kuu. Makao Makuu ya nchi lazima yawe na timu inayoshiriki ligi kuu na timu hiyo ni Dodoma FC ambayo tunatakiwa kuipa hamasa”, alisisitiza Rodney.

Aidha, Rodney aliupongeza uongozi wa Dodoma FC kwa kuitafutia timu hiyo michezo ya kujipima nguvu dhidi ya timu zinazoshiriki ligi kuu Tanzania bara. “Nilishuhudia mechi iliyopita baina ya Dodoma FC na Mbeya City ambapo timu hizo zilitoka sare tasa na leo nasubiri Dodoma FC itakapoivaa Lipuli FC kutoka Mkoa wa Iringa” alisema Rodney.

Kwa upande wake Afisa Habari wa Dodoma FC, Ramadhani Juma alisema kuwa mchezo wa leo dhidi ya ‘Wanapaluhengo’ Lipuli ya Iringa ni fursa kwa mashabiki na wadau wa Dodoma kwenda kujionea timu yao ikiwa imesukwa upya kwa ajili ya kujiwinda na ligi kuu daraja la kwanza inayotarajia kuanza hivi karibuni.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.