• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkurugenzi Kunambi awakaribisha wana Dodoma kuishangilia Dodoma Jiji FC

Imewekwa tarehe: February 7th, 2020

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi amewaomba  wajumbe wa kamati ya siasa  ya Mkoa ya  Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuhudhuria kwenye mechi ya ligi daraja la kwanza inayozikutanisha timu ya Dodoma Jiji FC dhidi ya Boma FC kutoka jijini Mbeya utakaochezwa  jumapili katika uwanja wa Jamhuri,  ili kuongeza hamasa kwa vijana na wananchi kwa ujumla kushiriki katika michezo.

Kunambi ameyasema hayo kwenye kituo cha maegesho ya malori Nala katika  ziara ya Kamati ya Siasa ya Mkoa ya CCM waliokuwa kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 43 ya chama hicho. Ziara hiyo  ilihusisha wilaya 7 na kuhitimishia katika Jiji la Dodoma  kwa kutembelea miradi ya kimkakati inayojengwa chini ya usimamizi wa  Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mkurugenzi Kunambi alisema vijana walioko katika timu inayomilikiwa na Jiji hilo, Dodoma Jiji FC wanajituma kwa hali na mali  katika kuinua soka jijini hapa ambapo timu inashika nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi  Daraja la Kwanza nchini.

“Hapa ni kituo cha maegesho ya magari makubwa ya mizigo ikiwa ni awamu ya kwanza ambapo katika ujenzi wa awamu ya pili tumejipanga kuongeza viwanja vya michezo ya mpira wa miguu na mpira wa kikapu, pia hosteli itakayotumika kwa ajili ya vijana wetu wa Dodoma Jiji FC, vyote vitajengwa pembezoni mwa kituo hiki .

“Hadi hivi sasa Dodoma Jiji FC ni kinara wa ligi ya daraja la kwanza, na siku ya jumapili itacheza katika uwanja wa Jamhuri hapa hapa nyumbani, niwaombe Mheshimiwa Mwenyekiti pamoja na wajumbe wote  mfike ili kuwapa 'sapoti' na kujionea uwezo wa vijana wetu wanaotuwakilisha vyema katika soka,” alisisitiza Kunambi.

Mkurugenzi huyo alisema siyo tu kwenye miradi ya kimkakati  bali Halmashauri ya jiji inafanya vyema hata katika upande wa michezo wako vizuri, na malengo yao kwa sasa ni  kufanya jitihada zitakazowezesha kuifikisha Dodoma Jiji FC katika ligi kuu ya Tanzania bara.

“Heshima kubwa tuliyopewa na mheshimiwa Rais John Magufuli ya kujenga uwanja wenye uwezo wa kuchukua watu laki moja kwa wakati mmoja, lazima tuwe na timu ambayo iko ligi kuu.

“Tunakwenda ligi kuu, Dodoma lazima tuwe na timu zaidi ya moja, hivyo tujitokeze kwa wingi uwanjani ili vijana wetu wapate morali ya kufanya vizuri zaidi katika uwanja wetu wa nyumbani,” alikazia MKurugenzi huyo.

Ziara hiyo jijini hapo imefanyika kwa siku mbili na kuongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya CCM, Mheshimiwa Godwin  Azaria Mkami wenye kaulimbiu  ya T tatu ikiwa ni Tumekagua, Tumejionea na Tumeridhishwa. Mwenyekiti alitoa mapendekezo hayo kwa  wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa katika mradi wa kimaendeleo wa ujenzi wa maegesho ya magari ya mizigo Nala.

Kikozi cha timu ya mpira wa miguu ya Dodoma Jiji FC kinachoongoza ligi daraja la kwanza nchini.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.