• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkurugenzi Mafuru aipongeza Chemicotex kuunga mkono elimu jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: September 17th, 2022
Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru ameipongeza Kampuni ya Chemicotex kwa kuchangia juhudi za halmashauri za kutokomeza daraja ziro kwa shule za sekondari katika matokeo mtihani wa taifa.

Kauli hiyo aliitoa leo ofisini kwake alipokutana na kufanya mazungumzo na Meneja wa Kampuni ya Chemicotex tawi la Dodoma Bi. Alice Joseph.

Mkurugenzi Mafuru alisema kuwa halmashauri yake inatumia bajeti kubwa katika utekelezaji mipango ya sekta ya elimu na itaendelea kutumia fedha nyingi ili kuifikisha elimu katika viwango vya juu. Alisema kuwa serikali pekee haitoshi, ushiriki wa wadau ni muhimu sana katika kufanikisha mipango ya elimu.

“Kampuni hii ya Chemicotex ni ya kwanza katika kuchangia program hii. Hivyo, niwaalike wadau wengine kuchangia sekta hii ili kwa pamoja tuisogeze mbele. Dodoma kuna watoto wengi wenye akili sana ila changamoto za kimazingira ndizo zinawakwamisha kuweza kufanya vizuri katika masomo yao” alisema Mkurugenzi Mafuru.

Akiongelea mchango wa wadau, alisema kuwa wadau wanamchango mkubwa katika kufanikisha mipango ya elimu. “Halmashauri tutapanga siku ili tuweze kukutana na wadau mbalimbali na kuwapa muelekeo na maono ya maendeleo ya halmashauri ili waweze kuchangia sekta ya elimu. Serikali hatutanyamaza, tutaendelea kutoa mchango wetu kwa ajili ya kukuza na kuendeleza sekta ya elimu” alisema Mkurugenzi Mafuru.

Akiongelea wanafunzi wanaoacha shule kutokana na sababu mbalimbali, alisema kuwa halmashauri itawatafuta na kuwarudisha shuleni. “Dodoma tuna ‘drop out’ ni lazima tuwatafute na kuwarudisha darasani ili tuwakomboe kielimu na kuwawezesha kuwa na mchango zaidi katika taifa lao” alisema Mkurugenzi Mafuru.

kwa upande wake Meneja wa Kampuni ya Chemicotex tawi la Dodoma, Alice Joseph alisema kuwa ameona inafaa kwa kampuni hiyo kutoa dawa za meno na miswaki kwa wanafunzi wote walio katika mpango wa tokomeza ziro katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Leo tunawakabidhi dawa za meno na miswaki ili muweze kufika mbali katika juhudi zenu za kutafuta elimu” alisema Alice.

Alisema kuwa kampuni yake inatamani kuona kiwango cha elimu kinapanda katika Jiji la Dodoma. Aliahidi kuendelea kushirikiana na jiji hilo katika kuinua masuala ya elimu.

Akimkaribisha Meneja wa Kampuni ya Chemicotex kukabidhi dawa za meno na miswaki kwa wanafunzi, Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Upendo Rweyemamu alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inatekeleza mkakati wa kutokomeza ziro katika kidato cha nne. “Tunafuraha leo hii kupokea ugeni toka Kampuni ya Chemicotex tawi la Dodoma. Awali tuliwasilisha mpango wa tokomeza ziro katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na leo wametuitikia na kutuletea vifaa hivi mnavyoviona hapa. Tunawashukuru sana kwa mchango wao” alisema Mwalimu Upendo.

Meneja wa Kampuni ya Chemicotex tawi la Dodoma, Alice Joseph (mbele) alipokuwa akiongea na vyombo vya habari.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.