• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkurugenzi Mafuru asifu matumizi ya TEHAMA

Imewekwa tarehe: August 6th, 2021

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru amepongeza matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kurahisisha mawasiliano na utendaji kazi baina ya waheshimiwa madiwani na timu ya menejimenti ya Halmashauri.

Pongezi hizo amezitoa leo katika mkutano wa mwaka wa Baraza la Madiwani alipokuwa akifafanua hoja zilizotolewa na madiwani katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Mipango jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mafuru alisema kuwa, ameona umuhimu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika kurahisisha ufanisi wa mawasiliano na utendaji kazi katika vikao. “…tumeona umuhimu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Mara ya mwisho nilisoma maswali na hoja 82 hapa mbele, na maswali hayo nilikuwa nayo mimi mwenyewe. Leo hii kila mjumbe ametumiwa maswali na majibu ya hoja katika kishikwambi” alisema Mkurugenzi Mafuru.

Akiongelea matumizi ya TEHAMA katika ufanisi wa kazi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano, Joseph Fungo alisema kuwa “Vishikwambi vimesaidia kurahisisha utendaji kazi, uendeshaji wa vikao na kukuza matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilinunua vishikwambi 100 kwa ajili ya Madiwani na Wataalam wake. Vishikwambi hivyo vimesaidia sana kupunguza matumizi ya shajara katika kutengeneza makabrasha na kupunguza gharama za uendeshaji wa vikao na mawasiliano;

Aidha, matumizi ya vishikwambi yamesaidia kurahisisha utaoji na ugawaji wa taarifa na makabrasha ya vikao kwa wakati na hivyo kuondoa zile gharama za matumizi ya magari na mafuta wakati wa kuyasambazia kwa Waheshimiwa Madiwani”.

Akifafanua zaidi alisema kuwa Madiwani na wataalam wanafurahia matumizi ya vishikwambi hivyo. “Kwa kweli tumeona wengi wao wanafurahia na wameweza kumudu matumizi yake kwa haraka. Hili linajidhihirisha kwa mabadiliko ya uendeshaji wa vikao vya Halmashauri. Sasa vikao vinaendeshwa kwa uwazi zaidi na kwa muda mfupi bila kuathiri ubora wa maamuzi na matokeo yake” alisema Fungo.

Naye Mhe. Aloyce Luhega, Diwani wa Kata ya Nzuguni, amesema kuwa “Wazo la matumizi ya vishikwambi kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni zuri kwa sababu vinatusaidia kupata taarifa mapema. Ni muhimu kwa sababu vinatusaidia kutunza kumbukumbu kwa urahisi kuliko tulivyokuwa tukitumia makabrasha. Utakumbuka tulikuwa na makabrasha makubwa kwa kikao kimoja jambo ambalo ilikuwa ni shida kwa ubebaji na uhifadhi wake, na unajua yakishakuwa mengi yanageuka kuwa uchafu;

Mimi nimefurahia matumizi ya vishikwambi na niipongeze sana Halmashauri yetu kwa uamuzi huo”. alimalizia Mhe. Luhega.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.