• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkurugenzi Mafuru awapa tumaini wakazi wa Nzuguni

Imewekwa tarehe: September 6th, 2020

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Joseph Mafuru ametoa wiki moja kuanzia Jumatatu ya tarehe 7 mpaka Ijumaa kwa wakazi wa Kata ya Nzuguni kusajili malalamiko na kero zao zinazohusu ardhi kwenye ofisi ya Mtendaji wa Mtaa wa Nzuguni ‘A’ ili maafisa wa ardhi wazichukue na kuzifanyia kazi.

Mafuru ameyasema hayo alipofanya ziara ya kikazi kwenye kata ya Nzuguni kwa lengo la kujitambulisha na kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili wakazi wa eneo hilo.

Alisema kuwa baada ya zoezi la kuorodhesha kero kukamilika,  siku ya Ijumaa mchana wataalam wa ardhi kutoka Halmashauri ya Jiji watazichukua ili kuzipitia na ifikapo Jumatatu ya tarehe 14 yeye pamoja na wakuu wa vitengo vinavyohusika na masuala ya ardhi na Mkuu wa Idara hiyo wataweka kambi katika ofisi ya Mtaa huo kwa siku tano ili kuzipitia kero hizo moja baada ya nyingine na kuzitatua.

“Baada ya zoezi la kusajili kero kukamilika, Jumatatu inayofuata nitafunga hema katika ofisi ya mtaa na nitahamisha wakuu wangu wa vitengo wote niliokuja nao hapa na mimi mwenyewe nikiwepo pamoja na mkuu wao wa Idara tutahamia hapo, tutaleta na gari tatu, kwa hiyo tutakua tunaangalia kero moja baada ya nyingine kama ni ya kwenda kuona tunaingia kwenye gari tunaenda kuangalia, tunatatua inaisha tunahamia kwa mtu mwingine” Alisema Mafuru.

Mbali na kero za migogoro ya ardhi wananchi wa kata hiyo pia walimuomba Mkurugenzi Mafuru kutatua kero za maji, umeme na barabara katika baadhi ya maeneo ndani ya kata hiyo.

Akijibu kuhusu kero ya umeme na maji Mafuru alisema, ataongea na wakuu wa Taasisi hizo ili kuona ni jinsi gani wanaweza kushirikiana kutatua kero hizo huku akiongeza kuwa kumekuwa na mahusiano mazuri kati yao hivyo kuwatoa hofu wananchi wa maeneo hayo kuwa kero hizo zitapatiwa ufumbuzi.

Akijibu kuhusu kero ya barabara mafuru alisema “tuna mitambo iliyoachwa na CDA, tuna greda tatu na mitambo mingine ambayo tumeona tuifufue ili kurahisisha zoezi la utengenezaji wa barabara kwasababu hapo mwanzo tulikua tunatumia gharama kubwa, wataalamu wetu wapo kazini na niwaambie tu kuwa baada ya wiki tatu mitambo hiyo itakua imepona na tutaanza zoezi hilo”.

Aidha Mafuru amewahakikishia wananchi hao kuwa kero zao zitatatuliwa na kila mmoja atapata haki yake, huku akiwaomba kuwa na imani na ofisi yake kwani wapo kwa ajili ya kuwatumikia.

Akifunga mkutano huo Mwenyekiti wa Mtaa huo alimshukuru Mkurugenzi na maafisa alioambatana nao kwa kuja kuwasikiliza na kuchukua kero zao.

Baadhi ya wakazi wa Nzuguni waliojitokeza kumsikiliza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru (hayupo pichani) katika ziara ya kujitambulisha na kutatua kero za wananchi.


Mkutano wa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na wananchi wa Nzuguni.


Baadhi ya wataalam wa Jiji la Dodoma walioambatana na Mkurugenzi wa Jiji wakisikiliza kwa makini wakati mkutano ukiendelea.


Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru (mwenye kipasa sauti) akiongea na wanachi wa Nzuguni (hawapo pichani) kushoto ni wataalam mbalimbali wa Jiji la Dodoma alioambatana nao.


Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru akifafanua kuhusu changamoto na utatuzi wake kwa wananchi wa Nzuguni.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.