• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkurugenzi Mafuru, timu yake wajipanga kutatua kero za ardhi Nzuguni 'A'

Imewekwa tarehe: September 12th, 2020

IDARA ya Mipango Miji, Ardhi na Maliasili katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma itaweka kambi ya siku tano kuanzia tarehe 14 Septemba, 2020 kutatua kero za ardhi kwa wananchi wa Mtaa wa Nzuguni “A” Kata ya Nzuguni kwa lengo la kuharakisha utoaji huduma na utendaji haki kwa wananchi.

Agizo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru (pichani juu) alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa za Nzuguni “A” uliopo Kata ya Nzuguni jijini hapa hivi karibuni.

Mkurugenzi Mafuru alisema kuwa Mtaa wa Nzuguni “A” una changamoto kubwa ya ardhi baada ya kupimwa na kurasimishwa. “Ndugu zangu nimekuja hapa kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi katika huu Mtaa wa Nzuguni “A”. Kila siku napokea karibu asilimia 80 ya barua za malalamiko ya ardhi kutoka eneo hili. Uamuzi wangu, nitaleta timu ya wataalam wa Idara ya Mipango Miji na Ardhi waje hapa waweke kambi kufuatilia kila mgogoro na kuutatua. Nitaleta gari tatu hapa, afisa anasikiliza mgogoro anaenda eneo la kiwanja kuona hali halisi na kuja na mapendekezo ya utatuzi wa mgogoro husika” alisema Mafuru. Nataka huduma itolewe kwa wananchi hapahapa ili wasipate usumbufu wa kuifuata huduma hiyo makao makuu, haki itatolewa hapahapa, aliongeza Mafuru.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Idara ya Mipango Miji, Ardhi na Maliasili, Emelye Chaula alisema kuwa maandalizi ya Idara yake kuweka kambi katika mtaa wa Nzuguni “A” yapo katika hatua nzuri. “Kesho Jumatatu tutaweka kambi eneo hilo kwa siku tano ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mkurugenzi wa Jiji. Kuwafuata wananchi katika maeneo yao na kutatua kero zao. Kambi hiyo itategemea na wingi wa watu. Tumeshajipanga na Afisa Mtendaji kuona namna bora ya kutoa huduma hiyo. Kama idadi ya watu itakuwa kubwa sana hatutasita kuongeza idadi ya siku ya kutoa huduma. Tunataka kila mwananchi atatuliwe kero yake” alisema Chaula.

Winifrida Bani ambaye ni mkazi wa Kata ya Nzuguni alisema kuwa ziara ya Mkurugenzi wa Jiji imewapunguzia kero ya kwenda Halmashauri ya Jiji kufuata huduma ya utatuzi wa migogoro ya ardhi katika kata yao. “Mimi nimempenda Mkurugenzi hasa alipoamua kuleta timu yake ya wataalam kuja Nzuguni kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi. Huyu baba kweli anawajali watu wa chini” alisema Bani.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.