• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkuu wa TEHAMA Jiji ataja faida mifumo

Imewekwa tarehe: September 21st, 2021

Na Sifa Stanley, DODOMA. 

MKUU wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari Mawasiliano na Uhusiano, (TEHAMA na Uhusiano) wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo amesema kuwa kitengo hicho kina mchango mkubwa katika kukuza mapato ya Halmashauri kupitia mifumo mbalimbali ya ukusanyaji wa kodi kwa njia ya kielektroniki.

Aliyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano maalum kuhusu kazi za kitengo hicho na umuhimu wake katika utendaji wa Halmashauri kwenye zama hizi zinazoshuhudia maendeleo makubwa ya Sayansi na Teknolojia ya Mawasiliano, ambapo mahojiano hayo yalifanyika katika ofisi za Halmashauri hiyo zilizopo mtaa wa CDA Jijini humo.

Mkuu huyo wa kitengo alisema kuwa, kitengo cha TEHAMA na Uhusiano kina mchango mkubwa katika kukuza mapato ya Halmashauri ya Jiji hilo kwa sababu malipo yote yanayofanyika hutumia mifumo ya TEHAMA.

“Mapato yote yanayokusanywa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma lazima yapite kwenye mfumo wa TEHAMA, tunatumia mfumo wa Wizara ya Fedha unaotumika kukusanya mapato ya Serikali (GePG), mfumo huo unasaidia kutoa namba ya malipo (control number) kwa ajili ya malipo na pia kuna mfumo ambao vyanzo vyote vya Halmashauri vinakusanywa kupitia mfumo wa Mapato ya ndani (LGRCIS) ambao licha ya kukusanya, umesaidia sana kudhibiti upotevu wa mapato” alisema Fungo.

Akiongelea juu ya namna kitengo kilivyojipanga katika mwaka wa fedha ulioanza Julai 2021 hadi Juni 2022, mkuu huyo alisema kuwa kitengo kimejipanga kufanya maboresho kwenye miundombinu na vifaa vya TEHAMA, ambayo yataendelea kuleta mabadiliko chanya katika halmashauri ya jiji na taifa kwa ujumla.

“Kwa mwaka huu wa fedha tumejipanga kufanya maboresho ya miundombinu, tutafanya maboresho ya vifaa, pia tutaimarisha miundombinu. Mifumo mingi inayotumika hapa haijatengenezwa na jiji, inatoka Wizara yetu ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa sehemu kubwa sisi ni kujiimarisha katika uboreshaji miundombinu pamoja na vifaa” alielezea Fungo.

Fungo alisema kuwa tayari katika kuhakikisha kuwa mianya ya upotevu wa mapato inadhibitiwa, Jiji limenunua vifaa vya kielektroniki vya kukusanyia mapato (Point of Sell Machines – POS) 292 ili kila chanzo kiwe inakusanywa bila kama ilivyokusudiwa katika Mpango na Bajeti ya Halmashauri.

Akiongelea kuhusu sehemu ya Habari, alisema kuwa wamejipanga kuhakikisha wanaongeza vitendea kazi vya kisasa ili kuboresha njia zinazotumika kutoa Habari, maudhui, picha za video na za mnato zihusuzo Halmashauri ya Jiji hususani miradi ya maendeleo na Habari zingine mbalimbali.

Ikumbukwe kuwa Jiji la Dodoma linamiliki kurasa za mitandao ya kijamii (Instagram, facebook), pia tovuti ya Jiji (www.dodomacc.go.tz), jarida linalotoka kila mwezi na televisheni ya mtandaoni (Dodoma City TV).

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.