• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma azindua kitabu cha Mwongozo wa mkakati wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji

Imewekwa tarehe: September 12th, 2022

Na. Josephine Kayugwa, DODOMA

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri amesema wanafunzi wanahitaji kusaidiwa kipindi cha mitihani kwa kuwa watulivu na kufundishwa uzalendo wakiwa shuleni kwa lengo la kuongeza ufaulu bila udanganyifu wowote.

Aliyasema hayo alipokuwa akizindua kitabu cha mwongozo wa mkakati wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya elimu msingi katika ukumbi wa mikutano wa shule ya msingi Mtemi Mzengo iliyopo katika Halmasahuri ya Jiji la Dodoma.

“Kitabu hiki cha mwongozo kitumike katika kuwafundishia wanafunzi, katika kipindi hiki cha mitihani watoto wanahitaji msaanda wenu kama walimu. Mnatakiwa kuwapa ushirikiano kwa kuwaelekeza taratibu na sheria za mitihani, tunataka Halmashuri ya Jiji la Dodoma iwe ya mfano katika suala la ufaulu kwa wanafunzi kiwango cha asilimia 87 kiongezeka zaidi katika matokeo yajayo,” alisema Shekimweri.

Aidha, aliongezea kuwa kila mtu ana wajibu wa kulipa kodi kwaajili ya kujenga miundombinu ya elimu ikiwemo shule bora ili kutoa elimu nzuri kwasababu idadi ya wanafunzi wanaosoma kwa sasa ni kubwa. “Serikali inaboresha madarasa na kununua vifaa vya kufundishia kupitia kodi, kwahiyo tuelimishane wote ili kutekeleza jambo hili,” alisema Shekimweri.

Kwa upande wake Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Myalla alisema kupitia mwongozo ambao umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, wana matarajio ya kuongeza ufaulu kwa madarasa yote ya mitihani.

“Katika kuongeza ufaulu kwa wanafunzi, tulianzisha vituo rekebishi kwaajili ya kuwasaidia kielimu kwa kuwaelekeza vitu vya muhimu na vyakuzingatia katika masomo na mitihani yao,” alisema Myalla.

Nae Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Mtemi Mazengo, Imani Weston alisema kuwa mkakati wa ufundishaji wa kuinua elimu ya msingi utasaidia ili kuweza kunyanyua kiwango cha elimu na kuwasaidia walimu katika ufundishaji.

“Ni kweli kama sisi walimu wakuu, waratibu elimu kata, maafisa elimu wa wilaya na walimu wenzetu kama wataitekeleza mikakati hii kwa sababui imefanyiwa utafiti wa kutosha ninaamini kabisa kiwango cha ufaulu katika shule zetu, kiwango cha ufaulu katika halmashauri yetu na taifa kwa ujumla kitapanda. Ufaulu utaongezeka sana kwa sababu mikakati imelenga changamoto zilizopo na namna ya kuzitatua ili kuinua kiwango cha elimu katika nchi yetu” alisema Weston.

Ikumbukwe kuwa kitabu cha mwongozo wa mkakati wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya elimu msingi ulizinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ufunguzi wa mashindano ya michezo ya shule za msingi (UMITASHUMTA) na mashindano ya michezo katika shule za sekondari (UMISSETA) Mkoani Tabora tarehe 4 Agosti, 2022.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.