• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mnaojenga Dodoma fuateni ramani zilizopitishwa - Jiji

Imewekwa tarehe: July 27th, 2020

WANANCHI wanaofanya ujenzi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamekumbushwa kuhakikisha majengo wanayojenga yanafuata michoro ya ramani iliyoidhinishwa na Jiji la Dodoma.

Ushauri huo umetolewa leo na Kaimu Mwenyekiti wa Timu Namba mbili ya Menejimenti ya Jiji la Dodoma Joseph Fungo iliyopita katika maeneo ya Swaswa na Ilazo Extention kufuatilia utekelezaji wa masharti ya ujenzi na kudhibiti ujenzi holela katika Jiji la Dodoma.

Fungo amesema kuwa ramani zinazopitishwa na Jiji la Dodoma zinakuwa zimekidhi masharti na vigezo na hivyo kuthibitishwa kuwa zinafaa kujengwa katika Jiji la Dodoma. "Katika ziara yetu tumegundua wako baadhi ya watu wana ramani zilizopitishwa na Jiji lakini majengo wanayojenga yako tofauti na ramani zilizopitishwa na Jiji, utaratibu ni kwamba kila mtu anatakiwa kujenga kama ramani iliyopitishwa inavyoonesha." amesisitiza Fungo.

Naye Mdhibiti wa Ujenzi holela wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Mhandisi Ally Bella amesema yeye na timu yake wataendelea kutekeleza majukumu yao kuhakikisha ujenzi ndani ya Jiji la Dodoma unafanyika kwa maelekezo ya michoro iliyopitishwa. Aidha, amewata watu wote wanaofanya ujenzi jijini Dodoma kuhakikisha kunakuwa na vibali vya ujenzi kwenye maeneo ya ujenzi (site).

"Tumejiandaa na kumejipanga kuhakikisha zoezi la udhibiti wa ujenzi holela hapa jijini linafanyika kwa mafanikio. Ukiacha Watendaji wa Kata, tunao watumishi wa Jiji ambao tumewagawa kwa kanda na jukumu lao ni kutembelea maeneo yao ili kuona shughuli za ujenzi zinazoendelea na kudhibiti ujenzi holela" alifafanua Mhandisi Bella.

Timu Namba mbili ya Menejimenti ya Jiji la Dodoma ikitembelea eneo la Ilazo Extension kudhibiti ujenzi holela jijini Dodoma.

Kaimu Mwenyekiti wa Timu namba mbili ya Menejimenti Joseph Fungo (kulia), Mkuu wa Udhibiti ujenzi holela wa Jiji la Dodoma Mhandisi Ally Bella (katikati) na mdhibiti ujenzi holela Abel Magehema (kushoto) wakiangalia ramani kuona kama ujenzi wa nyumba unaendana na ramani iliyopitishwa na Jiji.

 

Moja na ujenzi usiokidhi vigezo ambapo timu namba mbili ya menejimenti ilimtaka mwenye ujenzi huo kubomoa mara moja. Pichani askari wa Jiji akiweka agizo la kubomoa.


Hawa walikutwa wakijenga jengo ambalo haliko kwenye ramani na pia limeunganishwa kwenye uzio kitu ambacho ni kinyume na masharti ya ujenzi.

Timu namba mbili ya Menejimenti ya Jiji ikikagua ili kudhibiti ujenzi holela. 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.