• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mradi wa SGR Makutupora-Tabora, Tabora-Isaka kuanza karibuni

Imewekwa tarehe: September 5th, 2021

SHIRIKA la Reli Tanzania linategemea kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya kisasa - SGR kipande cha Makutupora – Tabora (KM 371) na Tabora – Isaka (KM 162), hivi karibuni ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Ujenzi wa SGR Makutupora hadi Isaka, ni muendelezo wa awamu ya kwanza ya ujenzi wa Reli ya Kisasa kutoka Dar es salaam hadi Mwanza yenye urefu wa Kilomita 1219, ambapo mpaka sasa utekelezaji wa awamu hiyo unafanyika katika vipande vitatu vya Dar es Salaam – Morogoro, Morogoro – Makutupora na Mwanza – Isaka ikiwa ni jumla ya Kilomita 1063 za njia kuu na njia za kupishania.

Akizungumza katika ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Tabora wakati wa ziara ya Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Reli Tanzania, Mkurugenzi mkuu wa TRC ndugu Masanja Kadogosa ameeleza kuwa taratibu za kuanza kwa utekelezaji wa mradi, Makutupora hadi Isaka zinaendelea vizuri, huku zikitarajiwa kukamilika hivi karibuni na ujenzi kuanza.

Kadogosa ameongeza kuwa “katika uendeshaji wa Reli, Tabora ni sehemu muhimu, treni zinazoenda Mpanda, Mwanza, Kigoma lazima zote zipite hapa kwahiyo ni eneo ambalo wanaliangalia sana.

Kadogosa aliongeza kuwa "Katika ujenzi wa Reli ya Kisasa, tutajitahidi kupita maeneo ya pembeni ya miji ili nyumba nyingi zisibomolewe, hapa Tabora Tutakuwa na Karakana na Stesheni kubwa”.

Aidha, kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi. Dkt. Batilda Buriani ameeleza kuwa huduma za reli zimekuwa chachu ya maendeleo ya wanatabora kwa miaka mingi na Kwamba wanatabora wako tayari na wana shauku kubwa ya kushuhudia kuanza rasmi kwa ujenzi wa vipande vya reli ya kisasa vya Makutupora – Tabora na Tabora - Isaka.

“Tuna imani kuwa kuanza kwa vipande hivi viwili vya mradi wa Ujenzi wa SGR, kutasisimua pia maeneo mengine katika mkoa wetu, kwahiyo niwahakikishie usalama na kuwa tutahakikisha hakuna hujuma zozote dhidi ya miundombinu hii inayojengwa kwa gharama kubwa” aliongeza Balozi. Dkt. Buriani.

Kwa upande Mwingine Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Reli Tanzania, Prof. John Kondoro amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora kufuatia ushirikiano wake kwa TRC na kwa kuhakikisha ulinzi na usalama wa miundombinu ya reli, aidha Prof. Kondoro ameahidi kuwa Shirika litaendelea kuhakikisha huduma nzuri za Reli na kufanyia kazi changamoto mbalimbali kwa maslahi ya watanzania.

Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Reli Tanzania ipo katika ziara ya Siku tatu mkoani Tabora hadi Mwanza Kukagua miundombinu ya reli pamoja na kipande cha tano cha Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa Mwanza – Isaka ambao umefikia 1% ya utekelezaji.

Chanzo: www.trc.co.tz

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.