• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Msigwa akabidhiwa ofisi, asisitiza uzalengo kwa Wanahabari

Imewekwa tarehe: April 16th, 2021

MKURUGENZI wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa, amesema kuwa atahakikisha anashirikiana na Waandishi wa habari kwa kuwapa taarifa zote wanazostahili kupata ili ziwafikie Wananchi kwa wakati.

Msigwa ameyasema hayo leo April 16, 2021 Jijini Dodoma wakati wa makabidhiano ya ofisi na mtangulizi wake ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sànaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbas.

Aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, leo amekabidhi kijiti hicho kwa Ndugu Gerson Msigwa aliyeteuliwa hivi karibuni na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan huku akikumbuka jinsi kazi hiyo ilivyomfanya asilale.

Dkt. Abbasi ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambapo, pamoja na kazi nyingine, ataendelea kuisimamia na kuisaidia ofisi hiyo ya Msemaji Mkuu, amewaambia waandishi wa habari Jijini Dodoma leo wakati wa makabidhiano kuwa kazi hiyo ilimchukua muda mwingi katika saa 24 za siku hivyo ni kazi adhimu na muhimu kwa Taifa.
Dkt. Abbasi amepongeza Bw. Msigwa kwa uteuzi huo na kueleza kuwa anaamini atafanikiwa kuendeleza pale yeye alipoishia.

Aidha, Dkt. Abbasi amemshukuru Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumwamini na kumteua mwaka 2016 na amemshukuru pia Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumuamini aendelee kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika uteuzi uliofanyika Aprili 4 mwaka huu.

Pia nawashukuru sana watanzania wote, wanahabari na wahariri wa vyombo vya habari tulioshirikiana katika kipindi chote cha uongozi wangu.
Kwa upande wake, Bw. Msigwa naye alimshukuru Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwa kumteua kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu kwa miaka mitano 5 na zaidi na sasa anamshukuru Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kumteua kwenye nafasi ya Msemaji Mkuu wa Serikali.

Vilevile, namshukuru Dkt. Hassan Abbasi kwa kunikabidhi rasmi ofisi leo na kwa kunipa ushirikiano mkubwa wakati nikiwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, ninaamini tuko pamoja hata kwenye majukumu haya mapya, amesema kuwa Dkt. Abbasi katika uongozi wake wa Usemaji Mkuu wa Serikali tayari amefyeka kichaka, na yeye sasa kazi yake ni kulima shamba ili kupata mazao mengi kwa maendeleo ya nchi yetu.

Msemaji  Mkuu wa Serikali huyo mpya ameweka wazi kuwa anatamani sana wanahabari wawe chachu ya kuleta mabadiliko, nchi yetu iwe ajenda ya kwanza, tuzingatie sheria, taratibu, kanuni na miongozo ili tuiweke nchi yetu mbele na kuyatangaza mazuri ya nchi yetu.

“Nitakuwa mtu wa mwisho katika kipindi cha uongozi wangu wa Msemaji Mkuu wa Serikali kuona waandishi wa habari tunatumia kalamu zetu kuibomoa Serikali na nchi yetu wenyewe ambayo tayari ilishapata uhuru. Nitahakikisha mnapata taarifa za shughuli zote zinazotekelezwa na Serikali mnazostahili kupata kama waandishi wa habari.”

Aidha, amesema kuwa ataweka mikakati jinsi ya kufanya kazi kwa kushirikiana na watendaji pamoja na wadau wa habari. Akamalizia kwa kumpongeza Dkt. Abbasi kwa kazi kubwa aliyoifanya na leo anakuwa bosi wake ni jambo la kumpongeza sana," alisema Msigwa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.