• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo atoa neno, maandalizi ya Uchaguzi Mkuu

Imewekwa tarehe: August 12th, 2020

WASIMAMIZI wasaidizi wa uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani mwaka 2020 ngazi ya Kata wametakiwa kutunza siri na kuimarisha mawasiliano baina yao na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo ili kuhakikisha uchaguzi mkuu unafanyika kwa ufanisi.

Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Dodoma Mjini, Wakili Msekeni Mkufya alipokuwa akiwasilisha mada ya wajibu, majukumu na mambo ya kuzingatiwa na wasimamizi wa uchaguzi katika ngazi ya kata katika mafunzo kwa wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma hivi karibuni.

Wakili Mkufya alisema kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo na kuwaelekeza mambo ya msingi wanayopaswa kuzingatia katika mchakato kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. “Mafunzo haya yanatolewa kwenu mkiwa kama wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata kuelekea uchaguzi huo, ambao utafanyika tarehe 28/10/2020. Tukumbuke kwamba, katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mchakato wa uchaguzi unatekelezwa kwa mujibu wa sheria, tukianza na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sheria ya uchaguzi sura ya 343 pamoja na kanuni za uchaguzi wa kiti cha Rais, Wabunge na Madiwani za mwaka 2020” alisema Wakili Mkufya.

Akiongelea mambo yanayopaswa kuzingatiwa na wasimamizi wasaidizi wakati wa kutekeleza majukumu yao, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Dodoma mjini alisema wanatakiwa kutunza siri. “Kutunza siri kwa maana ya kutokutoa taarifa za uchaguzi kwa mtu au mamlaka zisizohusika. Kuweka utaratibu mzuri wa kuwasiliana na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo, au wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi kuhusu mwenendo wa uchaguzi katika eneo lake” alisema msimamizi huyo.

Mambo mengine ni kuacha ushabiki wa chama chochote cha siasa katika kutekeleza majukumu yao na kufahamu mihemuko ya kisiasa katika eneo lake. Pia, “mnapaswa kukagua na kutembelea vituo vya uchaguzi vilivyopo katika maeneo yenu na mkibaini mapungufu ya vituo, mtafute namna bora ya kurekebisha kasoro hizo kwa kuwasiliana na Msimamizi wa Uchaguzi” aliongeza Wakili Mkufya.

Mambo mengine aliyoyasisitiza msimamizi huyo kwa wasimamizi wasaidizi ni kutetekeleza majukumu yao ya kusimamia uchaguzi kwa kuzingatia uadilifu na uaminifu kwa sababu kukosea ni kuichafua Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Kufanya jambo lolote kinyume na sheria na kanuni za uchaguzi ni kosa, kwa mujibu wa kifungu cha 98 cha sheria ya uchaguzi, aliongeza Wakili Mkufya.

Msimamizi huyo wa jimbo aliwataka wasimamizi wasaidizi kuepuka kufanya kazi kasipo kuzingatia sheria, kanuni na maelekezo kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi au msimamizi wa uchaguzi. Vilevile, aliwataka kuepuka kutokushirikisha msimamizi wa uchaguzi, wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi katika shughuli za uchaguzi katika eleo wanalosimamia.

Kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za mwaka 2020 zinaelekeza chini ya kanuni ya 13 (1) kwamba Tume ya Taifa ya uchaguzi inaweza kuchagua ana kuteua wasimamizi wasaidizi kutoka miongozi mwa watumishi wa umma ambao watakuwa na jukumu la kumsaidia msimamizi wa uchaguzi katika Jimbo na ngazi ya kata.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.