• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Neno la RC Mtaka kwa Ma-DC wapya Kongwa, Kondoa

Imewekwa tarehe: June 25th, 2021

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WAKUU wa Wilaya za Mkoa wa Dodoma wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa weledi na uzalendo hali wakitambua kuwa ni wasaidizi wa Rais katika wilaya zao.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka katika hafla fupi ya uapisho wa wakuu wa Wilaya wateule wa Mkoa wa Dodoma katika viunga vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa jijini Dodoma mapema wiki hii.

Mkuu wa Mkoa Mtaka alisema kuwa wakuu wa wilaya siyo wasaidizi wa Mkuu wa Mkoa bali ni wasaidizi wa Rais katika wilaya zao. “Mkijifanya ni wasaidizi wangu mtapotea.

Kila mmoja abebe thamani ya kumsaidia Rais katika wilaya yake. Hakikisheni mnatekeleza majukumu yenu kwa weledi na uzalendo mkubwa” alisema Mtaka.

Aidha, aliwapongeza wakuu wa wilaya hao kwa kuaminiwa na Rais katika nafasi hizo. Aliwataka kutambua kuwa vipaumbele katika mkoa ni elimu na viwanda. “Vipaumbele katika mkoa ni elimu na viwanda. Nendeni mkapime viwanja kwa ajili ya viwanda katika maeneo yenu. Tunataka kuitazama Dodoma katika miaka 20 ijayo tunataka kuona mabadiliko makubwa. Wekeni vivutio kwa wawekezaji ili waweze kuja kuwekeza katika maeneo yenu” alisema Mtaka.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Khamis Mkanachi alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumuamini na kumteua katika nafasi hiyo. Alisema kuwa kutokana na imahi hiyo atailipa kwa uwajibikaji. Akiongelea matarajio yake katika wilaya hiyo, alisema kuwa ni kuhakikisha huduma za kijamii zinakuwa bora. Aliahidi kusimamia utoaji bora wa huduma za Elimu, afya, maji, kilimo cha kisasa na uimarishaji wa uwekezaji katika sekta binafsi.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Remedius Emmanuel alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa imani aliyonayo kwake na kumuahidi ushirikiano. “Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, nikuahidi ushirikiano. Pia naomba ushirikiano wenu nyote. Kazi yangu kubwa kwenda kutekeleza imani ya Rais iliyoiweka kwa vijana inafikiwa katika Wilaya ya Kongwa” alisema Emmanuel.

Hafla hiyo ilitanguliwa na kiapo cha utii, wimbo wa Taifa, wimbo wa Afrika ya Mashariki, sala na dua na kiapo cha uadilifu kwa wateule, ilihudhuriwa na Kamati ya Usalama Mkoa, viongozi wa dini, wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wakiongozwa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru na wananchi.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.