• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mwanamke siyo mtu duni – Mhe. Tawfiq

Imewekwa tarehe: March 8th, 2021

WANANCHI wametakiwa kutambua kuwa Mwanamke siyo mtu duni wala chombo cha kudhalilishwa bali anatakiwa kupewa nafasi ili naye atoe mchango wake wa kimaendeleo kadri ya uwezo wake.

Hayo yamesemwa leo machi 8, 2021 na Mbunge wa Viti maalumu, Fatuma Toufiq alipokuwa akihutubia katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo yamefanyika kiwilaya katika kiwanja cha Nyerere square jijini Dodoma.

Toufiq amesema kuwa duniani kote wanawake wanafanya tathmini ya malengo ambayo wamejiwekea hususani katika kutetea haki mbalimbali za wanawake na kwamba Taifa linakabiliwa na changamoto nyingi zinazohitaji juhudi za makusudi katika kuzikabili na kwamba wenye kuweza kuzikabili changamoto hizo ni wanawake wenyewe.

Aidha, ameongeza kuwa mwanamke akipewa nafasi anaweza kwani mpaka sasa ni dhahiri wanawake waliopewa uongozi wanaweza kuongoza na kusimamia majukumu yao katika utekelezaji wa maendeleo mbalimbali.

Akifafanua zaidi, amesema kuwa kutokana na uelewa mdogo wa jamii umepelekea wanawake wengi kujiona wao si kitu si chochote lakini kutokana na juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali ya awamu ya tano imeweza kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo wanawake.

"nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa kumteua Makamu wa kwanza wa Rais mwanamke Mheshimiwa Samia Suluhu Hasan na kumwamini kuweza kuliongoza Taifa hili la Tanzania, hii yote ni kutimiza azma ya chachu ya kufikia Dunia yenye usawa kama ambavyo kauli mbiu ya siku ya wanawake inavyosema, nitoe rai kwa wanawake wote kutumia nafasi hii tuliyopewa katika kufanya mambo ya kimaendeleo na hasa katika kipindi hiki ambapo tayari Taifa letu lipo katika uchumi wa kati tutumie juhudi zetu na maarifa katika kuinua maendeleo yetu na hasa katika shughuli za ujasiliamali" alisema Toufiq.

Vilevile, amewataka wanawake wote kusimama imara katika kupiga vita ukatili wa kijinsia unaofanywa kwa watoto wa kike ikiwa ni pamoja na kukatishwa masomo kutokana na mimba za utotoni, kuozeshwa chini ya miaka 18, ukeketaji wa wanawake wakishirikiana na wanaume, vipigo kwa wanawake vinavyosbabishwa na jeuri ya fedha, hali inayopelekea kupoteza baadhi ya viungo na wakati mwingine kupata ulemavu wa kudumu na kupelekea mwanamke kuacha kutimiza ndoto zake.

"niwaombe wakina mama wenzangu tuongee na mabinti zetu wafahamu umuhimu wa elimu ya mimba na ndoa za utotoni, ninafahamu elimu imetolewa sana lakini tusichoke wamama sisi ndo tunajua thamani ya hawa mabinti zetu lakini pia tuendelee kuwafichua wale wote wanaowafanyia ukatili mabinti zetu ikiwa ni pamoja na kuwapa mimba wanafunzi ili waweze kuchukuliwa sheria stahiki" alisema Toufiq.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za idara ya maendeleo ya jamii jiji la Dodoma, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Sharifa Nabalang'anya amesema kuwa lengo la maadhimisho haya kwanza ni kutambua nafasi ya mwanamke katika jamii, pili kutoa fursa kwa wanawake, jamii na Vyama vya Siasa, Serikali na Asasi za kiraia kutafakari kwa undani mafanikio na changamoto mbalimbali zinazowakabili wanawake katika kujiletea maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Nabalang’anya amesema kuwa katika suala la kuwawezesha wanawake kiuchumi Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeweza kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa vikundi vya wanawake vilivyokidhi vigezo ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuondokana utegemezi.

Aidha katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021 Nabalang’anya amesema kuwa Halmashauri ya jiji la Dodoma imetenga kiasi cha shilingi 2,103,848,464.00 kwa ajili ya kutoa mikopo kupitia asilimia 10 ya makusanyo ya ndani ambapo vikundi vya wanawake vilivyokidhi vigezo vitakopeshwa shilingi 840,539,380.50 kupitia asilimia nne.






Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.