• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mwendazake JPM aagwa uwanja wa Bunge

Imewekwa tarehe: March 22nd, 2021

BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeishukuru Serikali kwa kuwapa nafasi ya kumuaga aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na ugumu wa ratiba.

Kauli hiyo imetolewa leo asubuhi na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai katika zoezi la kumuombea na kumuaga aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwenye uwanja wa Bunge la Tanzania.

Spika Ndugai amesema “tunaishukuru sana Serikali kwa kutupatia fursa hii ya kumuaga Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, pamoja na ratiba hii ngumu. Leo ni siku ya huzuni kubwa na majonzi makubwa. Tumechanganyikiwa, Watanzania wanalia, wamekata tamaa, lakini sisi wabunge tunasema asante Mungu kwa maisha ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, ambaye aliishi siku zote kwa kumtanguliza Mungu”.

Spika aliongeza kuwa wabunge wameondokewa na kiongozi, hasa akikumbuka mara ya mwisho alipoenda bungeni kutoa mtazamo wake kwa miaka mitano inayokuja kwa nchi ya Tanzania.

Alisema kuwa, Hayati Dkt. Magufuli aliweza kuhamisha Makao Makuu ya nchi kwenda Dodoma. “Naamini jambo hili litaendelezwa. Naamini Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege Msalato utekelezaji na ujenzi wa bomba la maji kutoka Ziwa Victoria utafika Dodoma katika kumuenzi Hayati Dkt. Magufuli” alielezea imani yake Spika Ndugai.

Aidha, alimtaja kuwa amejenga barabara, viwanja vya ndege, viwanda, shule, vituo vya afya, hospitali, bwawa la kufua umeme la Nyerere. “Umejenga, umejenga, umejenga. Hii ilikuwa mbegu ya kupanda. Sisi watanzania tutahakikisha tunaitunza na kumea” alisisitiza Spika Ndugai.

Akiongea kwa huzuni kubwa, waziri mkuu wa Tanzania, Kassim majaliwa amesema kuwa Hayati Dkt. Magufuli amefanya mambo mengi ambayo hayawezi kutajwa na kumalizika haraka. “Tunachokifanya hapa ni kumuombea. Nchi nzima imegubikwa na huzuni, Afrika Mashariki na SADC. Tunashuhudia viongozi wa nchi 17 wapo hapa kumuaga, kutokana na heshima ya kiongozi wetu” amesema Waziri Mkuu.

Kwa upande wake, Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akimuongelea hayati Dkt. Magufuli, alimtaja kuwa ndiye chimbuko lake kama Naibu Spika, alipomteua kuwa Mbunge na hatimae kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nae, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Zebeir Ali Maulid, amesema kuwa Hayati, Dkt. Magufuli atakumbukwa sana kwa kazi kubwa aliyofanya. Wingi wa watu waliojitokeza kumuaga Dar es Salaam na Dodoma ni dhihirisho kuwa alikuwa ni kiongozi wa watu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.