• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mwenge wa Uhuru waweka Jiwe la Msingi Kituo cha Afya Mkonze

Imewekwa tarehe: August 14th, 2019

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2019, Mzee Mkongea Ali ameridhishwa na maendeleo ya mradi wa kuboresha kituo  cha Afya Mkonze kwa kujenga majengo matano mapya ya Kituo hicho, baada ya ukaguzi mapema leo na kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa maboresho ya Kituo cha Afya.

Akiongea kabla ya kuweka jiwe la msingi, Ali alisema kuwa timu yake baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi katika Kituo cha Afya Mkonze, wamejiridhisha na ujenzi huo na kuweka jiwe la msingi. “Kituo kipo vizuri, na thamani ya fedha inaonekana. Hongereni sana” alisema Ali. Aliongeza kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiria kuimarisha afya za wananchi wake. Serikali imejenga vituo vya Afya 352 nchi nzima. Aidha, Serikali imeongeza bajeti ya dawa kwa Wizara ya Afya kutoka shilingi bilioni 1.9 hadi shilingi bilioni 2.2 mwaka huu” aliongeza Ali.

Akitoa ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, katika Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge alisema kuwa Mwenge wa Uhuru unalenga kuleta matumaini mahali ambapo hakuna matumaini, kuleta upendo mahali ambapo pana chuki na kuleta heshima mahali ambapo pana dharau.

Kiongozi huyo alisema kuwa ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 umejikita kwenye sekta ya Maji na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Aidha, aliwataka wananchi wenye sifa kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwaka huu.

Awali akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya mradi katika Kituo cha Afya Mkonze, Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho, Dkt. Baraka Chaula alisema kuwa mradi huo unahusisha ujenzi wa majengo matano, jengo la wodi ya wazazi, jengo la upasuaji, jengo la maabara, jengo la kuhifadhi maiti na nyumba ya mtumishi.
Dkt Chaula alisema kuwa mradi ulipata fedha kiasi cha shilingi 400,000,000 kutoka Serikali kuu kwa ajili ujenzi wa majengo yote matano mapya na “Mkurugenzi wa Jiji aliongezea kiasi cha shilingi 287,826,442 zikiwa ni gharama za kufunga mfumo wa kieletroniki wa uendeshaji na kukusanyia mapato, kujenga njia za watembea kwa miguu ambazo zitaunganisha majengo, kununua vifaa mbalimbali vya kumalizia ujenzi katika majengo yote matano, mfumo wa maji taka, malipo ya ufundi, ufungaji wa mfumo wa umeme – TANESCO, malipo ya mafundi ujenzi  wa kazi za ziada na ujenzi wa 'Incinarator'. Hivyo, mradi mzima utakapokamilika utagharimu kiasi cha Shilingi 687,826,442” alisema Dkt Chaula.

Mradi utakapokamilika utaongeza miundombinu mipya ya majengo, utoaji huduma za upasuaji wa dharura kwa akina mama wajawazito, kuboresha mazingira ya kutoa na kupata huduma ya afya kwa wananchi, aliongeza. ”Tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kutupa kipaumbele kuwa miongoni mwa vituo vya Afya 44 vya mwanzo kufanyiwa maboresho. Watumishi pamoja na wananchi wanafurahia kutoa na kupata huduma katika kituo hiki” alisema Dkt Chaula.
Ikumbukwe kuwa Kituo cha Afya Mkonze kilianzishwa tarehe 06/09/1993 kikiwa ni moja kati ya vituo vinne vya Afya vya Serikali vilivyopo katika Jiji la Dodoma.


Nyumba ya Mtumishi wa Kituo cha Afya ni miongoni mwa majengo ya mradi wa Maboresho ya Kituo cha Afya Mkonze.

Jengo la kuhifadhi maiti likiwa katika hatua za mwishoni kukamilika.

Jengo jipya la Maabara ya Kituo cha Afya Mkonze

Wadi ya Wazazi ya Kituo cha Afya Mkonze.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.