• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mwenge wazindua Shamba la Samaki kwa Pinda

Imewekwa tarehe: August 14th, 2019

WAZIRI mkuu mstaafu wa Tanzania, Mhe. Mizengo Peter Kayanza Pinda amepongeza utendaji kazi unaofanywa na Rais Dkt. John Magufuli katika mapambano dhidi ya rushwa na kurudisha nidhamu kwa watumishi wa umma nchini.


Pongezi hizo alizitoa alipokuwa akitoa salamu kufuatia Mwenge wa Uhuru kutembelea shamba lake eneo la Zuzu (Nzinje) kuzindua mradi wa ufugaji Samaki.

Pinda alisema ”shukrani kwa Rais Dkt John Magufuli kwa kazi kubwa anayofanya. Nimefanya kazi na tawala zote. Rais Magufuli ameonesha jeuri isiyo ya kawaida katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi. Katika utawala wake nidhamu imerudi kwa watendaji serikalini”. Maeneo mengine yaliyofanywa na Serikali hii aliyataja kuwa ni ujenzi wa mradi mkubwa wa bwawa la kufua umeme la Nyerere na reli ya kisasa ya umeme.

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, Mzee Mkongea Ali alimpongeza waziri mkuu mstaafu na kumuita mzalengo wa kweli. ”Katika eneo hili, watu mbalimbali wamekuwa wakija kujifunza shamba darasa bure, huu ni uzalengo wa kweli” alisema Ali. Kiongozi huyo Mzee Mkongea Ali amezindua rasmi Shamba hilo la Samaki katika eneo la Zuzu, Shamba linalomilikiwa na Pinda Farm Products ya Waziri Mkuu mstaafu Mhe. Mizengo Peter Kayanza Pinda.

Awali akiwasilisha taarifa ya mradi wa ufugaji Samaki katika shamba la Pinda, Mama Tunu Pinda alisema kuwa mradi wa ufugaji Samaki katika shamba la waziri mkuu mstaafu ni miongoni mwa miradi michache ya ufugaji Samaki iliyopo mkoani Dodoma, ukiwa na ujenzi wa mabwawa saba. Alisema kuwa mradi huo umegharimu shilingi milioni 29,500,000 kwa kujenga mabwawa saba.  

Akiongelea aina ya Samaki wanaozalishwa katika shamba hilo, alisema kuwa shamba hilo linazalisha Sato na Kambale. “Kwa upande wa Samaki aina ya Sato, bwawa dogo moja lina idadi ya Samaki kati ya 2,500 hadi 4,000. Bwawa kubwa lina idadi ya Samaki kati ya 8,000 hadi 10,000.  Kwa upande wa Samaki aina ya Kambale bwawa dogo linachukua Samaki 10,000 na bwawa kubwa linachukua Samaki 30,000. Mpaka sasa tumeshavua Samaki 1,800 kwa ajili ya kuuza awamu ya kwanza.  Jumla ya Samaki waliopo ni 6,000 Kambale pamoja na Sato. Kwa wastani bei ya Samaki ni shilingi 9,000 kwa kila kilo moja” alisema mama Pinda.

Mama Pinda aliendelea kusema kuwa ufugaji Samaki unakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa chakula cha Samaki cha uhakika kwa bei nafuu ndani ya nchi. ”Kwa sasa chakula kinachopatikana kinatengenezwa nje ya nchi  na kuuzwa kwa bei kubwa. Vifaranga vya samaki hupatikana maeneo ya mbali kama mto Ruvu ulioko Mkoa wa Pwani ambapo usafirishaji wake unakuwa mgumu mpaka kufika Dodoma vifaranga wengine wanakuwa wamechoka au wamekufa” alisema mama Pinda.


Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda akitoa maelezo kuhusu mabwawa ya Shamba la Samaki kwa wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2019.

Mandhari ya eneo la Shamba la Samaki la Mzee Mizengo Pinda.

Baadhi ya samaki aina ya sato wanaopatikana kwenye Shamba la Samaki linalomilikiwa na Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda Kayanza Pinda.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.