• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Naibu Waziri Mavunde awataka wadau wa kilimo kuzingatia mipango yao kwa vijana iendane na program ya BBT

Imewekwa tarehe: February 11th, 2023

NAIBU Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde amewataka wadau wote wa maendeleo ambao wanatekeleza miradi mbalimbali yenye lengo la kuvutia na kuinua vijana katika sekta ya kilimo kufuata muelekeo wa Programu ya Jenga Kesho iliyo Bora (Building a Better Tommorow - BBT) ili kuongeza wigo mpana zaidi wa kuwafikia vijana wengi.

Wito huo umetolewa Jijini Iringa na Naibu Waziri Mavunde aliposhiriki katika uzinduzi wa Mradi wa kuwawezesha Vijana na Wanawake katika mnyororo wa thamani wa kilimo awamu ya pili (Generation Food Accelerator II) chini ya ufadhili wa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya kupitia mradi wa Agri-connect.

"Ni dhahiri kwamba ninyi wadau, mkishirikiana na Serikali katika kutekeleza miradi yenu, kutaleta tija kubwa zaidi kutokana na kwamba, kutazuia upelekaji wa rasilimali fedha katika eneo hilo hilo moja kwa Serikali na wadau wa sekta binafsi.

Changamoto zinazowakabili vijana katika kilimo zinafahamika zikiwemo ukosefu wa ardhi, mitaji, pembejeo, miundombinu ya umwagiliaji na uhifadhi na masoko ya uhakika ya mazao watakayozalisha.

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya utashi wa kisiasa na mkazo mkubwa kwenye kilimo aliyouweka Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inakwenda kutatua changamoto hizo kupitia programu ya vijana ya _*Building a Better Tommorow *_kwa kuwatafutia ardhi na kuwamilikisha, kujenga miundombinu ya umwagiliaji na uhifadhi, kuwapatia pembejeo, kuwapa mitaji na kuwaunganisha na masoko ya uhakika.

Tunataka na ninyi wadau wote wa maendeleo ya masuala ya vijana kuhakikisha kwamba katika utekelezaji wa programu zenu mbalimbali mnazingatia mipango na muelekeo wa serikali katika kuwahudumia vijana kwenye sekta ya kilimo.

Nimefurahishwa na namna ambavyo mradi huo umepangwa kutekelezwa ambapo kiasi kikubwa cha fedha kitaelekezwa katika kuwapa vijana mitaji na ujenzi wa miundombinu, hali aliyoeleza kuwa uendelevu mkubwa kwa kijana hata pale ambapo mradi utafika mwisho,” alisema Mavunde

Awali, akitoa wasilisho, Mratibu wa mradi huo Ronald Mtana alieleza kuwa mradi huo ambao utawafikia vijana 30,000 wenye thamani ya Shilingi milioni 726 utatekelezwa kwa awamu katika Mikoa ya Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe na Katavi.

Katika hatua nyingine, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Uzalishaji Mazao kutoka Wizara ya Kilimo, Beatrice Banzi alieleza umuhimu wa sekta binafsi kuchangia jitihada za Serikali kutatua changamoto za vijana na kutoa wito kwa wadau wote wenye utayari kujiunga katika utekelezaji wa programu ya kuwezesha vijana kushiriki kilimo chenye tija.

Akitoa salamu zake, Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la RIKOLTO ambao ni sehemu ya watekelezaji wa mradi huo, Kein Mvanda aliishukuru Serikali kwa kuja na mradi wa BBT na kuahidi kuwa RIKOLTO itaendelea kutekeleza miradi na mipango yake kwa vijana kwa kufuata muelekeo na vipaumbele vya Serikali kupitia programu ya BBT.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.