• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

NAIBU WAZIRI JAFO ASISITIZA MATUMIZI YA MFUMO WA UENDESHAJI NA USIMAMIZI WA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

Imewekwa tarehe: October 5th, 2017

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ameutaka uongozi wa kituo cha Afya Makole kilichopo  manispaa ya Dodoma kuendelea kujizatiti katika matumizi ya mfumo wa uendeshaji na usimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya - GoTHoMIS ili kuboresha utoaji wa huduma na kudhibiti ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Mhe. Jafo ameyasema hayo wakati alipotembelea kituo cha Afya Makole kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali yaliyoelekeza ufungaji wa mifumo ya kielektroniki katika vituo vya kutolea huduma za Afya ili kuweka kumbukumbu ya taarifa zote za wagonjwa na sambamba na taarifa za fedha zinazotolewa na wagonjwa kuchangia huduma za Afya.

Mhe. Jafo amesema ameridhishwa na ufungaji na matumizi ya mfumo wa GoTHoMIS ambao kwa kiasi kikubwa unasaidia utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa na zaidi ya hapo kutunza taarifa zote za wagonjwa lakini mfumo huu haujatumika vizuri katika eneo la mapokezi ya fedha za uchangiaji wa huduma za Afya kwa sababu mapato ya kituo cha Makole hayajaongezeka kadiri inavyotakiwa.

Aliongeza kuwa "Mfumo huu ni mzuri sana katika uendeshaji na usimamaizi wa shughuli zinazotolewa katika vituo vya huduma za Afya, lakini sijaridhishwa na namna ambavyo mnautumia katika ukusanyaji wa mapato ya kituo cha Afya Makole".

Ninauhakika mfumo huu hamjautumia ipasavyo, haiwezekani mkakusanya shilingi milioni 9 kwa mwezi ingawa mapato yameongezeka kutoka shilingi milioni 3 mlizokuwa mnakusanya hapo awali ila ninauhakika mnaweza kukusanya zaidi ya kiasi hiki, hii ni kutokana na ukubwa wa kituo na idadi ya wagonjwa wanaotibiwa kwa siku.

Aliongeza kuwa "Kuwepo kwa mifumo ni jambo moja na kuutumia ipasavyo ni jambo lingine, jambo la msingi hapa ni uaminifu katika matumizi ya mifumo hii, kuna watu katika katika vituo hivi uaminifu ni mdogo hivyo husababisha kutoelewana baina ya wafanyakazi kwa kuwa sio wote wanaonufaika na udanganyifu huo lakini pia ni hasara kwa taifa".

Mhe. Jafo amewataka watumishi wa Makole kuongeza jitihada katika kuziba mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali na kuongeza uaminifu katika kila eneo linalohusu fedha za umma. Pia amewataka wataalam wa hospitali hiyo kufanya kazi kwa weledi na kutoa huduma stahiki kwa watumiaji wa kituo hicho na kuwataka kufuatilia fedha zilizotolewa na Serikali takribani milioni 500 kwa ajili ya ujenzi ya ukarabati kuhakikisha zinatumia pesa hizo kwa mujibu wa makubaliano katika uboreshaji wa vituo hivyo mpaka ifikapo 30 Disemba 2017.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.