• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Namba za Simu zilizojihusisha na Utapeli zafungiwa

Imewekwa tarehe: November 7th, 2022

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imebainisha kuwa maelfu ya namba za simu zilizojihusisha na wizi, utapeli na ulaghai kupitia Mtandao wa simu zimefungwa. 

Akizungumza jijini Dodoma hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Dkt Jabiri Bakari, alisema kuwa jumla ya namba tambulishi Hamsini na Mbili Elfu na Themanini na Saba 52,087 zikiwemo zilizoripotiwa kupotea, kuibiwa au kuhusika katika matukio ya kihalifu zimezuiliwa kupokea na kutoa huduma za Mawasiliano.

“Kwa mfano, Kuanzia Julai 2021 hadi kufikia Septemba 2022 jumla ya namba tambulishi (IMEI) zilizofungiwa na mfumo huu ni 52,087 ambazo ziliripotiwa kupotea, kuibiwa au kuhusika katika matukio ya kihalifu, hivyo kuwezesha kupunguza matukio ya wizi na kusaidia upatikanaji wa vifaa vya Mawasiliano vyenye ubora kwenye soko,” alisisitiza Dkt. Bakari.

Alieleza kuwa, kupitia kanzidata ya Namba Tambulishi (Central Equipment Identity Register), moduli hiyo imewezesha uhakiki wa vifaa vyote vinavyounganishwa na mitandao ya watoa huduma kama vinakidhi viwango vya kimataifa na ni salama kwa watumiaji.

Moduli hiyo iliyopo katika Mfumo wa Usimamizi wa Mawasiliano (TTMS) imewezesha kuzuia matumizi ya simu zilizoripotiwa kuibiwa, kupotea au kuharibika pamoja na kuzuia matumizi ya simu zisizokuwa na viwango.

“Usimamizi huu unawezesha kubaini na kufungia namba tambulishi za vifaa vya Mawasiliano zilizonakiliwa (Duplicate IMEIs), namba tambulishi za vifaa vilivyotumika kwenye udanganyifu pamoja na namba tambulishi zilizotolewa taarifa ya kupotea au kuibiwa,” aliongeza.

Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya wananchi akiwemo Mpoki Mwakabinga mkazi wa Kinondoni Dar es salaam waliishukuru Mamlaka ya Mawasiliano kwa jitihada inazofanya kuhakikisha uhalifu mtandaoni hasa unaohusisha vifaaa vya Mawasiliano kiganjani unatokomezwa kwa ushirikiano na vyombo vya ulinzi na Usalama.

“Tunaishukuru TCRA, hakika inajitahidi sana kuwalinda wananchi kupitia mifumo yake ya usimamizi wa Mawasiliano, hawa matapeli wamekuwa wengi kiasi kwamba tunakuwa na wasiwasi, kama wanafungiwa hili ni jambo la heri,” alibainisha Mpoki.

Mamlaka hiyo awali ilieleza kuwa watumiaji wa huduma za Mawasiliano ya simu mara wanapobaini kupokea simu au ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) wenye viashiria vya utapeli wanapaswa kutoa taarifa kwa kutuma ujumbe mfupi wenye neno “utapeli” kwenda namba 15040 na kutuma namba ya tapeli kwenda namba hiyohiyo.

Aidha TCRA ilisisitiza kila mtumiaji wa huduma za Mawasiliano ahakikishe anahakiki namba zake za simu zilizosajiliwa kwa njia ya kibayometria, kwa kutumia namba ya kitambulisho cha Taifa wanapaswa kubofya *106# kisha kufuata maelekezo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.